ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی * - لیست ترجمه ها

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

ترجمهٔ معانی سوره: سوره عبس   آیه:

Surat Abasa

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Alikunja kipaji na akageuka!
Uso wake ulitaghayari kwa kuchukia na akageuka,
تفسیرهای عربی:
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
Kwa sababu alimjia kipofu!
Kwa sababu kamjia kipofu anamuuliza khabari ya Dini yake.
تفسیرهای عربی:
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
Na wewe unajuaje, pengine huyo kipofu atatakasika kwa atayo yapata kwako,
تفسیرهای عربی:
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
Au atawaidhika na mawaidha yamfae.
تفسیرهای عربی:
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Ama ajionaye hana haja!
Ama yule anaye jiona ametosheka kwa mali yake na nguvu zake,
تفسیرهای عربی:
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
Wewe ndio unamshughulikia?
Wewe ndio unamkabili na unamshughulikia kumfikishia wito wako.
تفسیرهای عربی:
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na si juu yako kama hakutakasika.
Na wewe una lawama gani ikiwa yeye hakutakasika kwa Imani?
تفسیرهای عربی:
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama anaye kujia kwa juhudi .
Ama anaye kukimbilia kutafuta ilimu na uwongofu,
تفسیرهای عربی:
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
Naye anaogopa!
Naye anamkhofu Mwenyezi Mungu .
تفسیرهای عربی:
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
Ndio wewe unampuuza?
Wewe unampuuza.
تفسیرهای عربی:
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
Hakika Aya hizi ni mawaidha.
تفسیرهای عربی:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye penda akumbuke.
Mwenye kutaka atawaidhika kwa Qur'ani.
تفسیرهای عربی:
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
Nayo Qur'ani imo katika kurasa zilizo tukuzwa kwa Mwenyezi Mungu,
تفسیرهای عربی:
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
Zina cheo cha juu, na pahala palipo tukuka, zimetakasika na kila upungufu.
تفسیرهای عربی:
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
Katika mikono ya Malaika ambao Mwenyezi Mungu amewafanya ndio mabalozi baina yake na Mitume wake;
تفسیرهای عربی:
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Watukufu, wema.
Walio bora, wema.
تفسیرهای عربی:
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
Ameangamia mwanaadamu! Nini kilicho mfanya akufuru na hali Mwenyezi Mungu amemfanyia hisani zote hizi?
تفسیرهای عربی:
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwa kitu gani amemuumba?
Hakumbuki yeye kaumbwa kutokana na nini?
تفسیرهای عربی:
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
Kutokana na maji ya kudharauliwa Yeye Mwenyezi Mungu alimwanzisha kumuumba akamjaalia apitie daraja mbali mbali za kukua.
تفسیرهای عربی:
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha akamsahilishia njia.
Kisha akamfanyia nyepesi njia ya kufikia Imani, na akamfunza njia hiyo.
تفسیرهای عربی:
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
Kisha akamfisha na akamtukuza kwa kumtia kaburini.
تفسیرهای عربی:
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha apendapo atamfufua.
Na tena akipenda atamhuisha baada ya kufa kwake.
تفسیرهای عربی:
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
Ni kweli mwanaadamu, juu ya kuwa umri wake mrefu duniani, hakutimiza aliyo amrishwa na Mwenyezi Mungu katika mambo ya Imani na ut'iifu.
تفسیرهای عربی:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Hebu mtu na atazame chakula chake.
Hebu mtu na aangalie shani ya chakula chake - vipi tulivyo kipanga na kumsahilishia!
تفسیرهای عربی:
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
Ni Sisi tumeiteremsha mvua kutoka mbinguni, ikateremka.
تفسیرهای عربی:
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa ajili ya mimea.
تفسیرهای عربی:
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Kisha tukaotesha humo nafaka,
Tukaotesha humo nafaka ambazo watu huzila na huweka akiba.
تفسیرهای عربی:
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
Na zabibu, na mimea ya majani,
Na mizabibu na mimea ya majani inayo liwa mibichi.
تفسیرهای عربی:
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mizaituni, na mitende,
Na mizaituni mizuri, na mitende yenye kuzaa,
تفسیرهای عربی:
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
Na mabustani yaliyo songamana matawi ya miti yake,
تفسیرهای عربی:
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
Na matunda, na malisho ya wanyama;
Na matunda ya kustaladhi nayo, na malisha ya kula nyama hoa (mifugo).
تفسیرهای عربی:
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
Tumeotesha yote hayo kwa ajili ya faida yenu na wanyama wenu wa kufuga.
تفسیرهای عربی:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Basi utakapo kuja ukelele,
Basi utakapo kuja ukelele wa Kiyama utakao tia uziwi masikio,
تفسیرهای عربی:
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
Siku mtu atakapo mkimbia ndugu yake,
تفسیرهای عربی:
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Na mamaye na babaye,
Na mama yake, na baba yake,
تفسیرهای عربی:
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Na mkewe na wanawe.
Na mkewe, na wanawe!
تفسیرهای عربی:
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha
Kila mmojapo katika hawa atakuwa na jambo lake la kumshughulisha!
تفسیرهای عربی:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
Zipo nyuso siku hii zenye mwangaza,
تفسیرهای عربی:
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
Zitacheka, zitachangamka;
Zenye kung'ara na kufurahi kwa neema za Mwenyezi Mungu.
تفسیرهای عربی:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
Na nyuso nyengine siku hii zina vumbi zimesawijika.
تفسیرهای عربی:
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
Giza totoro litazifunika,
Zimegubikwa na kiza na weusi.
تفسیرهای عربی:
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao ndio makafiri watenda maovu
Wenye nyuso hizi ni makafiri wapotovu, ambao walio kuwa hawabali maasi waliyo kuwa wakiyatenda.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی سوره: سوره عبس
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی ـ ترجمهٔ علی محسن البروانی.

بستن