Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Sourate: ‘ABASA   Verset:

Surat Abasa

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Alikunja kipaji na akageuka!
Uso wake ulitaghayari kwa kuchukia na akageuka,
Les exégèses en arabe:
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
Kwa sababu alimjia kipofu!
Kwa sababu kamjia kipofu anamuuliza khabari ya Dini yake.
Les exégèses en arabe:
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
Na wewe unajuaje, pengine huyo kipofu atatakasika kwa atayo yapata kwako,
Les exégèses en arabe:
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
Au atawaidhika na mawaidha yamfae.
Les exégèses en arabe:
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Ama ajionaye hana haja!
Ama yule anaye jiona ametosheka kwa mali yake na nguvu zake,
Les exégèses en arabe:
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
Wewe ndio unamshughulikia?
Wewe ndio unamkabili na unamshughulikia kumfikishia wito wako.
Les exégèses en arabe:
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na si juu yako kama hakutakasika.
Na wewe una lawama gani ikiwa yeye hakutakasika kwa Imani?
Les exégèses en arabe:
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama anaye kujia kwa juhudi .
Ama anaye kukimbilia kutafuta ilimu na uwongofu,
Les exégèses en arabe:
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
Naye anaogopa!
Naye anamkhofu Mwenyezi Mungu .
Les exégèses en arabe:
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
Ndio wewe unampuuza?
Wewe unampuuza.
Les exégèses en arabe:
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
Hakika Aya hizi ni mawaidha.
Les exégèses en arabe:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye penda akumbuke.
Mwenye kutaka atawaidhika kwa Qur'ani.
Les exégèses en arabe:
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
Nayo Qur'ani imo katika kurasa zilizo tukuzwa kwa Mwenyezi Mungu,
Les exégèses en arabe:
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
Zina cheo cha juu, na pahala palipo tukuka, zimetakasika na kila upungufu.
Les exégèses en arabe:
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
Katika mikono ya Malaika ambao Mwenyezi Mungu amewafanya ndio mabalozi baina yake na Mitume wake;
Les exégèses en arabe:
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Watukufu, wema.
Walio bora, wema.
Les exégèses en arabe:
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
Ameangamia mwanaadamu! Nini kilicho mfanya akufuru na hali Mwenyezi Mungu amemfanyia hisani zote hizi?
Les exégèses en arabe:
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwa kitu gani amemuumba?
Hakumbuki yeye kaumbwa kutokana na nini?
Les exégèses en arabe:
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
Kutokana na maji ya kudharauliwa Yeye Mwenyezi Mungu alimwanzisha kumuumba akamjaalia apitie daraja mbali mbali za kukua.
Les exégèses en arabe:
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha akamsahilishia njia.
Kisha akamfanyia nyepesi njia ya kufikia Imani, na akamfunza njia hiyo.
Les exégèses en arabe:
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
Kisha akamfisha na akamtukuza kwa kumtia kaburini.
Les exégèses en arabe:
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha apendapo atamfufua.
Na tena akipenda atamhuisha baada ya kufa kwake.
Les exégèses en arabe:
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
Ni kweli mwanaadamu, juu ya kuwa umri wake mrefu duniani, hakutimiza aliyo amrishwa na Mwenyezi Mungu katika mambo ya Imani na ut'iifu.
Les exégèses en arabe:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Hebu mtu na atazame chakula chake.
Hebu mtu na aangalie shani ya chakula chake - vipi tulivyo kipanga na kumsahilishia!
Les exégèses en arabe:
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
Ni Sisi tumeiteremsha mvua kutoka mbinguni, ikateremka.
Les exégèses en arabe:
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa ajili ya mimea.
Les exégèses en arabe:
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Kisha tukaotesha humo nafaka,
Tukaotesha humo nafaka ambazo watu huzila na huweka akiba.
Les exégèses en arabe:
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
Na zabibu, na mimea ya majani,
Na mizabibu na mimea ya majani inayo liwa mibichi.
Les exégèses en arabe:
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mizaituni, na mitende,
Na mizaituni mizuri, na mitende yenye kuzaa,
Les exégèses en arabe:
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
Na mabustani yaliyo songamana matawi ya miti yake,
Les exégèses en arabe:
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
Na matunda, na malisho ya wanyama;
Na matunda ya kustaladhi nayo, na malisha ya kula nyama hoa (mifugo).
Les exégèses en arabe:
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
Tumeotesha yote hayo kwa ajili ya faida yenu na wanyama wenu wa kufuga.
Les exégèses en arabe:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Basi utakapo kuja ukelele,
Basi utakapo kuja ukelele wa Kiyama utakao tia uziwi masikio,
Les exégèses en arabe:
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
Siku mtu atakapo mkimbia ndugu yake,
Les exégèses en arabe:
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Na mamaye na babaye,
Na mama yake, na baba yake,
Les exégèses en arabe:
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Na mkewe na wanawe.
Na mkewe, na wanawe!
Les exégèses en arabe:
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha
Kila mmojapo katika hawa atakuwa na jambo lake la kumshughulisha!
Les exégèses en arabe:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
Zipo nyuso siku hii zenye mwangaza,
Les exégèses en arabe:
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
Zitacheka, zitachangamka;
Zenye kung'ara na kufurahi kwa neema za Mwenyezi Mungu.
Les exégèses en arabe:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
Na nyuso nyengine siku hii zina vumbi zimesawijika.
Les exégèses en arabe:
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
Giza totoro litazifunika,
Zimegubikwa na kiza na weusi.
Les exégèses en arabe:
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao ndio makafiri watenda maovu
Wenye nyuso hizi ni makafiri wapotovu, ambao walio kuwa hawabali maasi waliyo kuwa wakiyatenda.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Sourate: ‘ABASA
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture