Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany * - Tippudi firooji ɗii

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Firo maanaaji Simoore: Simoore Al-sarah   Aaya:

Surat Ash-Sharh

أَلَمۡ نَشۡرَحۡ لَكَ صَدۡرَكَ
Hatukukunjulia kifua chako?
Hakika tumekukunjulia kifua chako kwa kuwa tulitia ndani yake Uwongofu na Imani.
Faccirooji aarabeeji:
وَوَضَعۡنَا عَنكَ وِزۡرَكَ
Na tukakuondolea mzigo wako!
Na tumekupunguzia mizigo iliyo kuwa mizito juu ya mgongo wako, kwa kukuunga mkono na kukusahilishia mambo yako,
Faccirooji aarabeeji:
ٱلَّذِيٓ أَنقَضَ ظَهۡرَكَ
Ulio vunja mgongo wako?
Ambayo yalikuwa ni mazito juu ya mgongo wako.
Faccirooji aarabeeji:
وَرَفَعۡنَا لَكَ ذِكۡرَكَ
Na tukakunyanyulia utajo wako?
Na tumelitukuza jina lako, tukalifanya linatajwa na ulimi wa kila Muumini pamoja na jina letu.
Faccirooji aarabeeji:
فَإِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرًا
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi!
Hizo ni baadhi ya neema zetu juu yako. Basi kuwa na yakini na uweza wa Mwenyezi Mtukufu, kwani pamoja na uzito upo wepesi mwingi unao kuja nao.
Faccirooji aarabeeji:
إِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرٗا
Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
Hakika pamoja na uzito (wakati huo huo ijapo kuwa wewe hujui), upo wepesi mwingi vile vile.
Faccirooji aarabeeji:
فَإِذَا فَرَغۡتَ فَٱنصَبۡ
Na ukipata faragha, fanya juhudi.
Basi ukipata nafasi katika kazi ya kuwalingania watu, na mambo yaliyo khusiana na Jihadi, endelea na jitihada ya ibada na jishughulishe nafsi yako katika hayo.
Faccirooji aarabeeji:
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرۡغَب
Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.
Kwa Mola wako Mlezi tu ndio uelekee kwa kumwomba na kumhitajia.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simoore Al-sarah
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawahili, firi ɗum ko Ali Muhsin Al-barwani

Uddude