Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da yaren Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Sura: Suratu Al'qari'ah   Aya:

Surat Al-Qari'ah

ٱلۡقَارِعَةُ
Kiyama chenye kugonga nyoyo za watu kwa vituko vyake.
Tafsiran larabci:
مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Ni kitu gani hiko chenye kugonga?
Tafsiran larabci:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Na ni lipi lililokujulisha ni kipi hiko chenye kugonga?
Tafsiran larabci:
يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ
Siku hiyo watu watakuwa , kwa wingi wao, kugawanyika kwao na kuzunguka kwao, ni kama pandzi walioenea. Nao ni wale wanaojitupa motoni.
Tafsiran larabci:
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ
Na majabali yatakuwa ni kama pamba yenye rangi tofauti inayochambuliwa kwa mkono ikawa ni mapepe na ikamalizika.
Tafsiran larabci:
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi mwenye kuwa mizani za mema yake ni nzito,
Tafsiran larabci:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
atakuwa kwenye maisha ya kuridhika Peponi.
Tafsiran larabci:
وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Ama mwenye kuwa mizani za mema yake ni nyepesi na mizani za maovu yake ni nzito,
Tafsiran larabci:
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ
makazi yake yatakuwa ni Moto wa Jahanamu.
Tafsiran larabci:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ
Ni lipi lililokujulisha, ewe Mtume, ni ipi hii Jahanamu inayoitwa «Hāwiyah»?
Tafsiran larabci:
نَارٌ حَامِيَةُۢ
Ni Moto unaowaka sana kwa kuni ziliomo ndani yake.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Sura: Suratu Al'qari'ah
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da yaren Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Rufewa