Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs * - Lexique des traductions


Traduction des sens Sourate: AL-QÂRI’AH   Verset:

Surat Al-Qari'ah

ٱلۡقَارِعَةُ
Kiyama chenye kugonga nyoyo za watu kwa vituko vyake.
Les exégèses en arabe:
مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Ni kitu gani hiko chenye kugonga?
Les exégèses en arabe:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Na ni lipi lililokujulisha ni kipi hiko chenye kugonga?
Les exégèses en arabe:
يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ
Siku hiyo watu watakuwa , kwa wingi wao, kugawanyika kwao na kuzunguka kwao, ni kama pandzi walioenea. Nao ni wale wanaojitupa motoni.
Les exégèses en arabe:
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ
Na majabali yatakuwa ni kama pamba yenye rangi tofauti inayochambuliwa kwa mkono ikawa ni mapepe na ikamalizika.
Les exégèses en arabe:
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi mwenye kuwa mizani za mema yake ni nzito,
Les exégèses en arabe:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
atakuwa kwenye maisha ya kuridhika Peponi.
Les exégèses en arabe:
وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Ama mwenye kuwa mizani za mema yake ni nyepesi na mizani za maovu yake ni nzito,
Les exégèses en arabe:
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ
makazi yake yatakuwa ni Moto wa Jahanamu.
Les exégèses en arabe:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ
Ni lipi lililokujulisha, ewe Mtume, ni ipi hii Jahanamu inayoitwa «Hāwiyah»?
Les exégèses en arabe:
نَارٌ حَامِيَةُۢ
Ni Moto unaowaka sana kwa kuni ziliomo ndani yake.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Sourate: AL-QÂRI’AH
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs - Lexique des traductions

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Fermeture