Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Surah: Surah Al-Gāsyiyah   Ayah:

Surat Al-Ghashiyah

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ
Je, ilikujia,ewe Mtume, habari ya Kiyama chenye vituko venye kuwaenea watu?
Tafsir berbahasa Arab:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Nyuso za Makafiri, Siku hiyo, zitakuwa zimenyongeka kwa adhabu.
Tafsir berbahasa Arab:
عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ
Zishughulishie, zimechoka na kutaabika.
Tafsir berbahasa Arab:
تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ
Zinachomwa kwa Moto wenye kuwaka kwa ukali.
Tafsir berbahasa Arab:
تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ
Zitanyweshwa maji ya chemchemi yenye moto sana.
Tafsir berbahasa Arab:
لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ
Watu wa Motoni hawatakuwa na chakula isipokuwa kinachotoka kwenye mti wa miba ilioshikana na chini. Ni kibaya sana chakula hiko na ni kichafu mno.
Tafsir berbahasa Arab:
لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ
Hakimnoneshi mwenye kukila, awapo amekonda, wala hakimuondolei njaa, awapo na njaa.
Tafsir berbahasa Arab:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ
Nyuso za Waumini, siku ya Kiyama, zitakuwa kwenye neema.
Tafsir berbahasa Arab:
لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ
Kwa kuwa zilijishughulisha ulimwenguni kumtii Mwenyezi Mungu na kuridhika na Akhera.
Tafsir berbahasa Arab:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Zitakuwa kwenye Pepo ya daraja ya juu.
Tafsir berbahasa Arab:
لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ
Hutasikia humo hata neno moja la upuuzi.
Tafsir berbahasa Arab:
فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ
Ndani yake kuna chemchemi yenye kuteremka maji yake.
Tafsir berbahasa Arab:
فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ
Ndani yake mna vitanda vilioangatika,
Tafsir berbahasa Arab:
وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ
na vikombe vilivyotayarishwa kwa wenye kunywa,
Tafsir berbahasa Arab:
وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ
na mito iliyopangwa, mmoja baada ya mwingine,
Tafsir berbahasa Arab:
وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ
na mazulia mengi yaliyotandikwa.
Tafsir berbahasa Arab:
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ
Kwani, hawa makafiri wenye kukanusha, hawaangalii ngamia namna walivyoumbwa kiajabu?
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ
Na mbingu namna zlizoinuliwa juu kwa namna ya kupendeza?
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ
Na milima namna iliyoimarishwa ukapatikana uthabiti na utulivu wa ardhi?
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ
Na ardhi namna ilivyotandikwa na kutayarishwa?
Tafsir berbahasa Arab:
فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ
Basi wawaidhie, ewe Mtume, wale wenye kupa nyongo yale uliyotumilizwa kwayo wala usihuzunike kwa kupa mgongo kwao.
Tafsir berbahasa Arab:
لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ
Kwani wewe ni muwaidhiaji kwao, na si juu yako kuwalazimisha kuamini..
Tafsir berbahasa Arab:
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini yule mwenye kuyapa mgongo makumbusho na mawaidha na akawa mkakamavu kwenye ukafiri wake,
Tafsir berbahasa Arab:
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ
Mwenyezi Mungu Atamuadhibu adhabu kali Motoni.
Tafsir berbahasa Arab:
إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ
Hakika wao watarudi kwetu baada ya kufa.
Tafsir berbahasa Arab:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم
Kisha ni juu yetu kuwalipa kwa waliyoyafanya.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Surah: Surah Al-Gāsyiyah
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Terjemahan makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke bahasa Sawahili oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis

Tutup