Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs * - Lexique des traductions


Traduction des sens Sourate: AL-GHÂCHIYAH   Verset:

Surat Al-Ghashiyah

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ
Je, ilikujia,ewe Mtume, habari ya Kiyama chenye vituko venye kuwaenea watu?
Les exégèses en arabe:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Nyuso za Makafiri, Siku hiyo, zitakuwa zimenyongeka kwa adhabu.
Les exégèses en arabe:
عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ
Zishughulishie, zimechoka na kutaabika.
Les exégèses en arabe:
تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ
Zinachomwa kwa Moto wenye kuwaka kwa ukali.
Les exégèses en arabe:
تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ
Zitanyweshwa maji ya chemchemi yenye moto sana.
Les exégèses en arabe:
لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ
Watu wa Motoni hawatakuwa na chakula isipokuwa kinachotoka kwenye mti wa miba ilioshikana na chini. Ni kibaya sana chakula hiko na ni kichafu mno.
Les exégèses en arabe:
لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ
Hakimnoneshi mwenye kukila, awapo amekonda, wala hakimuondolei njaa, awapo na njaa.
Les exégèses en arabe:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ
Nyuso za Waumini, siku ya Kiyama, zitakuwa kwenye neema.
Les exégèses en arabe:
لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ
Kwa kuwa zilijishughulisha ulimwenguni kumtii Mwenyezi Mungu na kuridhika na Akhera.
Les exégèses en arabe:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Zitakuwa kwenye Pepo ya daraja ya juu.
Les exégèses en arabe:
لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ
Hutasikia humo hata neno moja la upuuzi.
Les exégèses en arabe:
فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ
Ndani yake kuna chemchemi yenye kuteremka maji yake.
Les exégèses en arabe:
فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ
Ndani yake mna vitanda vilioangatika,
Les exégèses en arabe:
وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ
na vikombe vilivyotayarishwa kwa wenye kunywa,
Les exégèses en arabe:
وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ
na mito iliyopangwa, mmoja baada ya mwingine,
Les exégèses en arabe:
وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ
na mazulia mengi yaliyotandikwa.
Les exégèses en arabe:
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ
Kwani, hawa makafiri wenye kukanusha, hawaangalii ngamia namna walivyoumbwa kiajabu?
Les exégèses en arabe:
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ
Na mbingu namna zlizoinuliwa juu kwa namna ya kupendeza?
Les exégèses en arabe:
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ
Na milima namna iliyoimarishwa ukapatikana uthabiti na utulivu wa ardhi?
Les exégèses en arabe:
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ
Na ardhi namna ilivyotandikwa na kutayarishwa?
Les exégèses en arabe:
فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ
Basi wawaidhie, ewe Mtume, wale wenye kupa nyongo yale uliyotumilizwa kwayo wala usihuzunike kwa kupa mgongo kwao.
Les exégèses en arabe:
لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ
Kwani wewe ni muwaidhiaji kwao, na si juu yako kuwalazimisha kuamini..
Les exégèses en arabe:
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini yule mwenye kuyapa mgongo makumbusho na mawaidha na akawa mkakamavu kwenye ukafiri wake,
Les exégèses en arabe:
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ
Mwenyezi Mungu Atamuadhibu adhabu kali Motoni.
Les exégèses en arabe:
إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ
Hakika wao watarudi kwetu baada ya kufa.
Les exégèses en arabe:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم
Kisha ni juu yetu kuwalipa kwa waliyoyafanya.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Sourate: AL-GHÂCHIYAH
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs - Lexique des traductions

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Fermeture