Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Surah: Soerat Al-Ghaasjijah (Het Overweldigende Evenement)   Vers:

Surat Al-Ghashiyah

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ
Je, ilikujia,ewe Mtume, habari ya Kiyama chenye vituko venye kuwaenea watu?
Arabische uitleg van de Qur'an:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Nyuso za Makafiri, Siku hiyo, zitakuwa zimenyongeka kwa adhabu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ
Zishughulishie, zimechoka na kutaabika.
Arabische uitleg van de Qur'an:
تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ
Zinachomwa kwa Moto wenye kuwaka kwa ukali.
Arabische uitleg van de Qur'an:
تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ
Zitanyweshwa maji ya chemchemi yenye moto sana.
Arabische uitleg van de Qur'an:
لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ
Watu wa Motoni hawatakuwa na chakula isipokuwa kinachotoka kwenye mti wa miba ilioshikana na chini. Ni kibaya sana chakula hiko na ni kichafu mno.
Arabische uitleg van de Qur'an:
لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ
Hakimnoneshi mwenye kukila, awapo amekonda, wala hakimuondolei njaa, awapo na njaa.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ
Nyuso za Waumini, siku ya Kiyama, zitakuwa kwenye neema.
Arabische uitleg van de Qur'an:
لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ
Kwa kuwa zilijishughulisha ulimwenguni kumtii Mwenyezi Mungu na kuridhika na Akhera.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Zitakuwa kwenye Pepo ya daraja ya juu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ
Hutasikia humo hata neno moja la upuuzi.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ
Ndani yake kuna chemchemi yenye kuteremka maji yake.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ
Ndani yake mna vitanda vilioangatika,
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ
na vikombe vilivyotayarishwa kwa wenye kunywa,
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ
na mito iliyopangwa, mmoja baada ya mwingine,
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ
na mazulia mengi yaliyotandikwa.
Arabische uitleg van de Qur'an:
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ
Kwani, hawa makafiri wenye kukanusha, hawaangalii ngamia namna walivyoumbwa kiajabu?
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ
Na mbingu namna zlizoinuliwa juu kwa namna ya kupendeza?
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ
Na milima namna iliyoimarishwa ukapatikana uthabiti na utulivu wa ardhi?
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ
Na ardhi namna ilivyotandikwa na kutayarishwa?
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ
Basi wawaidhie, ewe Mtume, wale wenye kupa nyongo yale uliyotumilizwa kwayo wala usihuzunike kwa kupa mgongo kwao.
Arabische uitleg van de Qur'an:
لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ
Kwani wewe ni muwaidhiaji kwao, na si juu yako kuwalazimisha kuamini..
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini yule mwenye kuyapa mgongo makumbusho na mawaidha na akawa mkakamavu kwenye ukafiri wake,
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ
Mwenyezi Mungu Atamuadhibu adhabu kali Motoni.
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ
Hakika wao watarudi kwetu baada ya kufa.
Arabische uitleg van de Qur'an:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم
Kisha ni juu yetu kuwalipa kwa waliyoyafanya.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Surah: Soerat Al-Ghaasjijah (Het Overweldigende Evenement)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman - Index van vertaling

De vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Dr. Abdullah Mohammed Abu Bakr en Sheikh Naser Khamis.

Sluit