Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Isura: Alghashiyat (Igitwikira)   Umurongo:

Surat Al-Ghashiyah

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ
Je, ilikujia,ewe Mtume, habari ya Kiyama chenye vituko venye kuwaenea watu?
Ibisobanuro by'icyarabu:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Nyuso za Makafiri, Siku hiyo, zitakuwa zimenyongeka kwa adhabu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ
Zishughulishie, zimechoka na kutaabika.
Ibisobanuro by'icyarabu:
تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ
Zinachomwa kwa Moto wenye kuwaka kwa ukali.
Ibisobanuro by'icyarabu:
تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ
Zitanyweshwa maji ya chemchemi yenye moto sana.
Ibisobanuro by'icyarabu:
لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ
Watu wa Motoni hawatakuwa na chakula isipokuwa kinachotoka kwenye mti wa miba ilioshikana na chini. Ni kibaya sana chakula hiko na ni kichafu mno.
Ibisobanuro by'icyarabu:
لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ
Hakimnoneshi mwenye kukila, awapo amekonda, wala hakimuondolei njaa, awapo na njaa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ
Nyuso za Waumini, siku ya Kiyama, zitakuwa kwenye neema.
Ibisobanuro by'icyarabu:
لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ
Kwa kuwa zilijishughulisha ulimwenguni kumtii Mwenyezi Mungu na kuridhika na Akhera.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Zitakuwa kwenye Pepo ya daraja ya juu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ
Hutasikia humo hata neno moja la upuuzi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ
Ndani yake kuna chemchemi yenye kuteremka maji yake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ
Ndani yake mna vitanda vilioangatika,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ
na vikombe vilivyotayarishwa kwa wenye kunywa,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ
na mito iliyopangwa, mmoja baada ya mwingine,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ
na mazulia mengi yaliyotandikwa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ
Kwani, hawa makafiri wenye kukanusha, hawaangalii ngamia namna walivyoumbwa kiajabu?
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ
Na mbingu namna zlizoinuliwa juu kwa namna ya kupendeza?
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ
Na milima namna iliyoimarishwa ukapatikana uthabiti na utulivu wa ardhi?
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ
Na ardhi namna ilivyotandikwa na kutayarishwa?
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ
Basi wawaidhie, ewe Mtume, wale wenye kupa nyongo yale uliyotumilizwa kwayo wala usihuzunike kwa kupa mgongo kwao.
Ibisobanuro by'icyarabu:
لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ
Kwani wewe ni muwaidhiaji kwao, na si juu yako kuwalazimisha kuamini..
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini yule mwenye kuyapa mgongo makumbusho na mawaidha na akawa mkakamavu kwenye ukafiri wake,
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ
Mwenyezi Mungu Atamuadhibu adhabu kali Motoni.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ
Hakika wao watarudi kwetu baada ya kufa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم
Kisha ni juu yetu kuwalipa kwa waliyoyafanya.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Isura: Alghashiyat (Igitwikira)
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga