Na walitaka kukukera ili uitoke nchi. Na hapo wao wasingeli bakia humo ila kwa muda mchache tu. [76]
[76] Na makafiri wa Makka wamejaribu, na walikaribia kukuudhi mpaka wakutoe kwenye ardhi ya Makka kwa uadui wao na chuki zao. Na lau yangeli kuwa hayo, basi wao nao wasingeli baki humo ila muda mchache tu, kisha washindwe katika hayo mambo yao, na hukumu iwe ya Mwenyezi Mungu.
Shika Swala jua linapo pinduka mpaka giza la usiku, na Qur'ani ya al fajiri. Hakika Qur'ani ya alfajiri inashuhudiwa daima. [78]
[78] Shika Swala zilizo faridhiwa, tangu kupinduka jua kati ya mbingu kuelekea upande wa machwea jua, mpaka kiza cha usiku. Na hizi ndizo Swala za Adhuhuri, Alasiri, Magharibi na Isha. Na pia shika Swala ya Alfajiri ambayo wanaishuhudia Malaika.
Na amka usiku kwa ibada; ni ziada ya sunna khasa kwako wewe. Huenda Mola wako Mlezi akakunyanyua cheo kinacho sifika. [79]
[79] Na katika wakati wa usiku amka, kwa kusali Swala ya Tahajjud. Hiyo ni ibada ya zaidi juu ya zile Swala Tano. Hii imekukhusu wewe tu, kwa kutaraji kuwa Mola wako Mlezi atakuweka Siku ya Kiyama makamo watakao kusifia viumbe.
Na sema: Mola wangu Mlezi! Niingize muingizo mwema, na unitoe kutoka kwema. Na unipe nguvu zinazo toka kwako zinisaidie. [80]
[80] Na sema: Ewe Mola Mlezi! Niingize maingizo ya kuridhisha matukufu katika kila unapo niingiza katika jambo au pahala. Na unitoe kwa kutoka kunako ridhisha kutukufu. Na kwa fadhila yako nijaalie nguvu za kunisaidia niwashinde maadui zangu.
Na sema: Kweli imefika, na uwongo umetoweka. Hakika uwongo lazima utoweke! [81]
[81] Na sema ukiwaonya watu wako washirikina: Haki ya Tawhid, Imani ya Mungu Mmoja, na Dini ya Kweli na Uadilifu, imekwisha fika. Na uwongo, na ushirikina, na dini ya ufisadi na dhulma, yote hayo yameondoka. Kwani uwongo daima hauna dawamu.
Na tunateremsha katika Qur'ani yaliyo ni matibabu na rehema kwa Waumini. Wala hayawazidishii madhaalimu ila khasara. [82]
[82] Na vipi Haki isiwe na nguvu na hali Sisi tunateremsha katika Qur'ani dawa ya kuponyesha maradhi ya shaka katika vifua vya watu, na sababu za kuwapatia rehema wanao iamini! Na madhaalimu hawana linao wazidia ila khasara tu kwa kuikataa kwao.
Na mwanaadamu tunapo mneemesha hugeuka na kujitenga kando. Na inapo mgusa shari hukata tamaa. [83]
[83] Na hakika katika maumbile ya mwanaadamu ni kujidanganya na kukata tamaa. Tukimneemesha kwa kumpa uzima na ukunjufu wa mali, hupuuza kutukumbuka na kutuomba, na hujitenga nasi kwa kiburi na majivuno! Na akiguswa na shari, kama ugonjwa na ufakiri, huwa mwingi wa kukata tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu.
Na mwanaadamu tunapo mneemesha hugeuka na kujitenga kando. Na inapo mgusa shari hukata tamaa. [84]
[84] Ewe Nabii! Waambie makafiri wa Kikureshi kwa kuepuka kuchochea ugomvi na makindano: Kila mmoja wetu na mmoja wenu anatenda na anakwenda kwa kufuata njia yake. Na Mola wenu Mlezi ni Mjuzi mno, wala hana ajuaye kuliko Yeye kumjua nani aliye shika njia sawa na kufuata Haki. Na huyo humlipa ujira wake kaamili. Na kumjua aliye potea njia, na huyo humpa adhabu kama anayo stahiki.
Na wanakuuliza khabari za Roho. Sema: Roho ni katika mambo ya Mola wangu Mlezi. Nanyi hamkupewa katika ilimu ila kidogo tu. [85]
[85] Ewe Muhammad! Watu wako wanakuuliza kwa kutomezwa na Mayahudi: Nini hakika ya Roho? Waambie: Roho ni katika ilimu yake Mwenyewe Mola wangu Mlezi aliyo jikhusisha nayo Yeye. Na nyinyi hamkupewa ilimu ila chache tu ukilinganisha na ilimu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Na tungeli penda tungeli yaondoa tuliyo kufunulia. Kisha usingeli pata mwakilishi wa kukupigania kwetu kwa haya. [86]
[86] Na lau tungeli taka kuifuta kabisa kifuani mwako hiyo Qur'ani tuliyo kufunulia tungeli fanya hivyo, na kisha usingeli mpata yeyote wa kukunusuru katika watu wako.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
លទ្ធផលស្វែងរក:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".