Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis * - Vertimų turinys


Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Al- ʻAadijaat   Aja (Korano eilutė):

Surat Al-Aadiyat

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa farasi wenye kwenda shoti katika njia Yake kumkabili adui, wakitoa sauti kwa kasi ya kukimbia. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Tafsyrai arabų kalba:
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wenye kutoa cheche za moto kwa kwato zao ngumu wanapokimbia kwa kasi.
Tafsyrai arabų kalba:
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wenye kushambulia maadui kipindi cha asubuhi.
Tafsyrai arabų kalba:
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Wakarusha vumbi kwa mbio zao.
Tafsyrai arabų kalba:
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Wakautia kati, kwa kuuzunguka kwa vipando vyao, mkusanyiko wa maadui.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika binadamu ni mkanushaji sana neema za Mola wake.
Tafsyrai arabų kalba:
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na yeye anakubali ukanushaji wake.
Tafsyrai arabų kalba:
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Na yeye ana pupa sana la mali.
Tafsyrai arabų kalba:
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani binadamu hajui linalomngojea mbele yake, pindi Mwenyezi Mungu Atakapowatoa wafu makaburini waende kuhesabiwa na kulipwa?
Tafsyrai arabų kalba:
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na (kwani yeye hajui) yakatolewa yaliyo ndani ya vifua: mema au maovu?.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Hakika Mola wao kwao na kwa amali zao, Siku Hiyo, ni Mtambuzi; hakuna chenye kufichamana Kwake.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Al- ʻAadijaat
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Dr. Abdullah Muchammed Abu Bakr ir šeichas Naser Khamis.

Uždaryti