Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis * - Índice de tradução


Tradução dos significados Surah: Suratu At-Tariq   Versículo:

Surat At-Tariq

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu na nyota yenye kuchomoza usiku.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ
Na ni lipi lilokujulisha ni ukubwa gani wa nyota hiyo?
Os Tafssir em língua árabe:
ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ
Hiyo ni nyota ing’arao na kuzagaa.
Os Tafssir em língua árabe:
إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ
Hakuna nafsi yoyote isipokuwa amewakilishwa kwayo Malaika mwenye kuchunguza na kusjili amali zake ili ihesabiwe Siku ya Kiyama.
Os Tafssir em língua árabe:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Basi aangalie binadamu mwenye kukanusha kufufuliwa ameumbwa kwa kitu gani? Ili ajue kuwa kurudisha umbo lake mara ya pili si vigumu kama kuumbwa mara ya kwanza.
Os Tafssir em língua árabe:
خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ
Aliumbwa kwa manii yenye kupenyeza ndani ya uzao kwa haraka.
Os Tafssir em língua árabe:
يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yatokayo kwenye mgongo wa mwnamume na kifua cha mwanamke.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ
Hakika yule Aliyemuumba binadamu kwa maji haya ni muweza wa kumrudisha kwenye uhai baada ya kufa.
Os Tafssir em língua árabe:
يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ
Siku zitakapofunuliwa wazi siri ziliofichwa na nafsi na kupambanuliwa njema na mbovu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ
Binadamu hatakuwa na nguvu ya kuitetea nafsi yake wala hatakuwa na mtetezi wa kumwepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ
Na Anaapa kwa mbingu yenye mvua ya kukaririka.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلۡأَرۡضِ ذَاتِ ٱلصَّدۡعِ
Na ardhi yenye pasuko za kufanya mimea ichipuke.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلٞ فَصۡلٞ
Hakika Qur’ani ni neno lenye kupambanua baina ya haki na batili.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَا هُوَ بِٱلۡهَزۡلِ
Na si upuuzi. Haifai kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Akifanya hivyo atakuwa amemshirikisha Mwenyezi Mungu.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّهُمۡ يَكِيدُونَ كَيۡدٗا
Hakika wenye kumkanusha Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani wanafanya vitimbi na mipango ili kuipinga haki na kuitilia nguvu batili.
Os Tafssir em língua árabe:
وَأَكِيدُ كَيۡدٗا
Na Mimi nafanya vitimbi kuidhihirisha haki ingawa makafiri wanatukia.Usiwe na haraka nao, ewe Mtume, kutaka wateremshiwe adhabu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَمَهِّلِ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَمۡهِلۡهُمۡ رُوَيۡدَۢا
Wape muhula uwangojee muda mchache wala usiwafanyie haraka, utaona adhabu itakayowafikia, mateso na maangamivu.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Surah: Suratu At-Tariq
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão em suaíli pelo Dr. Abdalla Mohamed Abubakar e Nassor Khamis

Fechar