Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Mealler fihristi


Anlam tercümesi Sure: Sûretu'ş-Şems   Ayet:

Surat Ash-Shams

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa jua na mchana wake na mwangaza wake wa asubuhi.
Arapça tefsirler:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapolifuata wakati wa kucha na kutwa.
Arapça tefsirler:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapoliondoa giza na kulifunua.
Arapça tefsirler:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا
Na kwa usiku unapoifinika ardhi ikawa giza.
Arapça tefsirler:
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kujengeka kwake kiimara.
Arapça tefsirler:
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kutandikika kwake.
Arapça tefsirler:
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa kila nafsi na namna Mwenyezi Mungu alivyoikamilisha umbo lake ili itekeleze kazi iliyoumbiwa nayo.
Arapça tefsirler:
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا
Akaibainishia njia ya shari na njia ya kheri.
Arapça tefsirler:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Amefaulu mwenye kuisafisha na kuikuza kwa kheri.
Arapça tefsirler:
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na ameingia kwenye hasara mwenye kuitia nafsi yake kwenye maasia.
Arapça tefsirler:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ
Kabila la Thamūd lilimkanusha Nabii wake kwa kuvama kwenye uasi.
Arapça tefsirler:
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا
Pindi walipotoka wabaya zaidi wa kabila hilo kumchinja Ngamia. Mtume wa Mwenyezi Mungu’ Ṣāliḥ, amani imshukie,
Arapça tefsirler:
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا
akawaambia: «Tahadharini kumgusa kwa ubaya ngamia ambaye ni miujiza ilioletwa na Mwenyezi Mungu kwenu inayoonyesha ukweli wa Nabii wenu, na msizuie kinywaji chake. Yeye ana siku yake ya kunywa na nyinyi mna siku yenu maalumu ya kunywa.» Hilo likawa zito kwao.
Arapça tefsirler:
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا
Wakamkanusha na kulipuza onyo lake wakamchinja.Mola wao Akawafinika kwa adhabu, akaisawazisha juu yao na hakuna aliyeweza kuponyoka.
Arapça tefsirler:
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا
Wala Haogopi, Mwenye uwezo uliotukuka, athari ya adhabu kali Aliywateremshia.
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Sure: Sûretu'ş-Şems
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Mealler fihristi

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Kapat