د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه سورت: الشمس   آیت:

Surat Ash-Shams

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa jua na mchana wake na mwangaza wake wa asubuhi.
عربي تفسیرونه:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapolifuata wakati wa kucha na kutwa.
عربي تفسیرونه:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapoliondoa giza na kulifunua.
عربي تفسیرونه:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا
Na kwa usiku unapoifinika ardhi ikawa giza.
عربي تفسیرونه:
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kujengeka kwake kiimara.
عربي تفسیرونه:
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kutandikika kwake.
عربي تفسیرونه:
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa kila nafsi na namna Mwenyezi Mungu alivyoikamilisha umbo lake ili itekeleze kazi iliyoumbiwa nayo.
عربي تفسیرونه:
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا
Akaibainishia njia ya shari na njia ya kheri.
عربي تفسیرونه:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Amefaulu mwenye kuisafisha na kuikuza kwa kheri.
عربي تفسیرونه:
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na ameingia kwenye hasara mwenye kuitia nafsi yake kwenye maasia.
عربي تفسیرونه:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ
Kabila la Thamūd lilimkanusha Nabii wake kwa kuvama kwenye uasi.
عربي تفسیرونه:
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا
Pindi walipotoka wabaya zaidi wa kabila hilo kumchinja Ngamia. Mtume wa Mwenyezi Mungu’ Ṣāliḥ, amani imshukie,
عربي تفسیرونه:
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا
akawaambia: «Tahadharini kumgusa kwa ubaya ngamia ambaye ni miujiza ilioletwa na Mwenyezi Mungu kwenu inayoonyesha ukweli wa Nabii wenu, na msizuie kinywaji chake. Yeye ana siku yake ya kunywa na nyinyi mna siku yenu maalumu ya kunywa.» Hilo likawa zito kwao.
عربي تفسیرونه:
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا
Wakamkanusha na kulipuza onyo lake wakamchinja.Mola wao Akawafinika kwa adhabu, akaisawazisha juu yao na hakuna aliyeweza kuponyoka.
عربي تفسیرونه:
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا
Wala Haogopi, Mwenye uwezo uliotukuka, athari ya adhabu kali Aliywateremshia.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه سورت: الشمس
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس - د ژباړو فهرست (لړلیک)

په سواهیلي ژبه کې د قرآن کریم د معناګانو ژباړه، د ډاکټر عبدالله محمد ابوبکر او شیخ ناصر خمیس لخوا ژباړل شوی.

بندول