የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አሽ ሸምስ   አንቀጽ:

Surat Ash-Shams

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa jua na mchana wake na mwangaza wake wa asubuhi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapolifuata wakati wa kucha na kutwa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapoliondoa giza na kulifunua.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا
Na kwa usiku unapoifinika ardhi ikawa giza.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kujengeka kwake kiimara.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kutandikika kwake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa kila nafsi na namna Mwenyezi Mungu alivyoikamilisha umbo lake ili itekeleze kazi iliyoumbiwa nayo.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا
Akaibainishia njia ya shari na njia ya kheri.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Amefaulu mwenye kuisafisha na kuikuza kwa kheri.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na ameingia kwenye hasara mwenye kuitia nafsi yake kwenye maasia.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ
Kabila la Thamūd lilimkanusha Nabii wake kwa kuvama kwenye uasi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا
Pindi walipotoka wabaya zaidi wa kabila hilo kumchinja Ngamia. Mtume wa Mwenyezi Mungu’ Ṣāliḥ, amani imshukie,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا
akawaambia: «Tahadharini kumgusa kwa ubaya ngamia ambaye ni miujiza ilioletwa na Mwenyezi Mungu kwenu inayoonyesha ukweli wa Nabii wenu, na msizuie kinywaji chake. Yeye ana siku yake ya kunywa na nyinyi mna siku yenu maalumu ya kunywa.» Hilo likawa zito kwao.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا
Wakamkanusha na kulipuza onyo lake wakamchinja.Mola wao Akawafinika kwa adhabu, akaisawazisha juu yao na hakuna aliyeweza kuponyoka.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا
Wala Haogopi, Mwenye uwezo uliotukuka, athari ya adhabu kali Aliywateremshia.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አሽ ሸምስ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዶ/ር ሙሐመድ ዓብደሏህ አቡ በክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ

መዝጋት