Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Isura: Asham’s (Izuba)   Umurongo:

Surat Ash-Shams

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa jua na mchana wake na mwangaza wake wa asubuhi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapolifuata wakati wa kucha na kutwa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapoliondoa giza na kulifunua.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا
Na kwa usiku unapoifinika ardhi ikawa giza.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kujengeka kwake kiimara.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kutandikika kwake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa kila nafsi na namna Mwenyezi Mungu alivyoikamilisha umbo lake ili itekeleze kazi iliyoumbiwa nayo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا
Akaibainishia njia ya shari na njia ya kheri.
Ibisobanuro by'icyarabu:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Amefaulu mwenye kuisafisha na kuikuza kwa kheri.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na ameingia kwenye hasara mwenye kuitia nafsi yake kwenye maasia.
Ibisobanuro by'icyarabu:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ
Kabila la Thamūd lilimkanusha Nabii wake kwa kuvama kwenye uasi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا
Pindi walipotoka wabaya zaidi wa kabila hilo kumchinja Ngamia. Mtume wa Mwenyezi Mungu’ Ṣāliḥ, amani imshukie,
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا
akawaambia: «Tahadharini kumgusa kwa ubaya ngamia ambaye ni miujiza ilioletwa na Mwenyezi Mungu kwenu inayoonyesha ukweli wa Nabii wenu, na msizuie kinywaji chake. Yeye ana siku yake ya kunywa na nyinyi mna siku yenu maalumu ya kunywa.» Hilo likawa zito kwao.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا
Wakamkanusha na kulipuza onyo lake wakamchinja.Mola wao Akawafinika kwa adhabu, akaisawazisha juu yao na hakuna aliyeweza kuponyoka.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا
Wala Haogopi, Mwenye uwezo uliotukuka, athari ya adhabu kali Aliywateremshia.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Isura: Asham’s (Izuba)
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga