የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አን ነበእ   አንቀጽ:

Surat An-Naba

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
Kuhusu kitu gani baadhi ya makafiri wa Kikureshi wanaulizana?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ
Wanaulizana kuhusu habari iliyo na uzito mkubwa kabisa,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ
nayo ni Qur’ani tukufu inayotoa habari za kufufuliwa ambako makafiri wa Kikureshi wana shaka nako na wanakukanusha.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Mambo sivyo kama wanavyodhania hawa washirikina. Hapo watajua hawa washirikina upeo wa kukanusha kwao na kitawadhihirikia waziwazi kile Atakachowatenda Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Kisha litahakikishika kwao jambo hilo na utahakikishika kwao ukweli wa yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kuhusu Qur’ani na kufufuliwa. Huu ni utisho na makemeo kwao.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا
Kwani hatukuwatandazia ardhi kama tandiko?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا
Na Tukawafanyia majabali kuwa ni vigingi, ili isitisike nanyi?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا
Na Tukawaumba aina mbali-mbali, mume na mke.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا
Na Tukafanya usingizi wenu ni mapumziko kwa viwiliwili vyenu: ndani yake mnatulia na kupumzika?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا
Na Tukaufanya usiku kuwa ni vazi, unawavisha giza lake na kuwafinika, kama nguo inavyomsitiri mwenye kuivaa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا
Na Tukaufanya mchana ni kipindi cha kutafuta maisha, mnaenea humo kwa ajili ya maisha yenu na mnatembea humo kwa ajili ya maslahi yenu?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا
Na Tukajenga juu yenu mbingu saba, madhubuti jengo lake, lilioumbwa kwa uzuri, halina mapasuko wala nyufa?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا
Na Tukalifanya jua kuwa ni taa iwakayo na kung’ara?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا
Na Tukateremsha kutoka kwenye mawingu yanyeshayo maji yamiminikayo kwa wingi,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا
ili Tutoe kwa maji hayo nafaka inayoliwa na watu,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَجَنَّٰتٍ أَلۡفَافًا
nyasi zinazoliwa na wanyama na miti iliyosongamana kwa kutawanyika tagaa zake?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا
Hakika Siku ya Uamuzi kati ya viumbe,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا
nayo ni Siku ya Kiyama, imekuwa ni wakati na ahadi iliyowekewa muda maalimu kwa watu wa mwanzo na wa mwisho.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا
Na zikafunguliwa mbingu zikawa ni zenye milango mingi kwa ajili ya kuteremka Malaika.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا
Na yakalipuliwa majabali baada ya kuwa yamekita, yakawa ni kama mangati.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا
Hakika Jahanamu, Siku Hiyo, itawalindiza wenye ukafiri ambao Moto huo umeandaliwa wao.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابٗا
Kwa makafiri ndio marejeo.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا
Watabakia humo muda mrefu ufuatanao, usiokoma.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا
Hawatakula humo chochote kitakachozizimisha joto la moto kwao.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا
Wala kinywaji kitakachowaondolea kiu yao. Isipokuwa maji moto na usaha wa watu wa motoni.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
جَزَآءٗ وِفَاقًا
Watakuwa wanalipwa kwa hilo malipo ya sawa yanayolingana na vitendo vyao walivyovitenda duniani
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا
Hakika wao walikuwa hawaiyogopi Siku ya Hesabu, na kwa hivyo hawakujitayarisha nayo kwa kufanya matendo ya kuwafaa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا
Na waliyakanusha waziwazi yaliyoletwa na Mitume.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا
Na kila kitu Tulikijua na Tukakiandika katika Ubao uliohifadhiwa (Al-Lawḥ Al-Maḥfūd).
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا
Basi Onjeni, enyi makafiri, hayo yakiwa ni malipo ya vitendo vyenu, Hatutawazidishia isipokuwa adhabu juu ya adhabu yenu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika kwa wale ambao wanamuogopa Mola wao na huku wanatenda mema kuna kufaulu kwa kuingia Peponi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا
Hakika watapata Mabustani makubwa na zabibu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا
Na watapata wanawake wenye umri mdogo, wenye vifua vilivyojaza, marika na waume zao.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا
Na watapata glasi zlizojaa pombe.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّٰبٗا
Hawatasikia katika Pepo hiyo maneno ya upotofu wala kudanganyana.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا
Watayapata yote hayo yakiwa ni malipo na zawadi na kipewa kingi cha kuwatosha kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلرَّحۡمَٰنِۖ لَا يَمۡلِكُونَ مِنۡهُ خِطَابٗا
Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati ya hizo, Mwenye kuwarehemu duniani na Akhera. Hawataweza kumuomba isipokuwa kile walichopewa ruhusa kumuomba.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا
Siku atakaposimama Jibrili na Malaika wengine hali ya kujipanga mlolongo. Hawatamuombea isipokuwa yule aliyetolewa ruhusa na Mwingi wa Rehema ya kuombewa na akasema maneno ya haki na ya sawa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo siku ya haki isiyokuwa na shaka kuja kwake. Kwa hivyo, yule atakaye kuokoka na vituko vya Siku hiyo, na ajifanyie njia ya marejeo kwa Mola wake kutenda vitendo vyema.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّآ أَنذَرۡنَٰكُمۡ عَذَابٗا قَرِيبٗا يَوۡمَ يَنظُرُ ٱلۡمَرۡءُ مَا قَدَّمَتۡ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلۡكَافِرُ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ تُرَٰبَۢا
Sisi Tunawaonya nyinyi adhabu ya Siku ya mwisho iliyo karibu. Siku ambayo atayaona kila mtu aliyoyatenda katika kheri au aliyoyachuma miongoni mwa madhambi. Na kafiri atasema, kwa kitisho cha Hesabu, «Laiti mimi nilikuwa mchanga na sikufufuliwa.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አን ነበእ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዶ/ር ሙሐመድ ዓብደሏህ አቡ በክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ

መዝጋት