للإطلاع على الموقع بحلته الجديدة

ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني سورة: الضحى   آية:

سورة الضحى - Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Naapa kwa mchana! [1]
[1] Naapa kwa wakati wa kupanda juu jua, na ni wakati wa uchangamfu na kazi!
التفاسير العربية:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapo tanda! [2]
[2] Na naapa kwa usiku unapo tulia na ukatanda kote kiza chake!
التفاسير العربية:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe. [3]
[3] Ewe Muhammad! Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukuchukia.
التفاسير العربية:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia. [4]
[4] Na matokeo ya mambo yako, mwisho wake, yatakuwa bora kuliko mwanzo wake.
التفاسير العربية:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike. [5]
[5] Na ninaapa kuwa bila ya shaka hapo Mola wako Mlezi atakupa kheri za duniani na Akhera hata utaridhia.
التفاسير العربية:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi? [6]
[6] Kwani hakukukuta wewe yatima unahitaji wa kukutunza naye akakupa makaazi ya kukuhifadhi kwa mwenye kukuangalia vyema kwa mambo yako?
التفاسير العربية:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea akakuongoa? [7]
[7] Na akakuona umebabaika hukukinaika na itikadi zilizo kuzunguka, naye akakuongoa kwenye Njia ya Haki?
التفاسير العربية:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza? [8]
[8] Akakukuta fakiri wa mali naye akakutajirisha kwa kukupa riziki?
التفاسير العربية:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimwonee! [9]
[9] Ikiwa hii ndiyo hali yetu nawe, basi yatima usimdhili,
التفاسير العربية:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie! [10]
[10] Na mwenye kuomba au kuuliza usimjibu kwa ukavu,
التفاسير العربية:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie. [11]
[11] Na ama neema za Mola wako Mlezi zitangaze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa ndio kudhihirisha neema.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني سورة: الضحى
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق