Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Capítulo: Sura Ad-Dhuhaa   Versículo:

Surat Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Naapa kwa mchana!
Naapa kwa wakati wa kupanda juu jua, na ni wakati wa uchangamfu na kazi!
Las Exégesis Árabes:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapo tanda!
Na naapa kwa usiku unapo tulia na ukatanda kote kiza chake!
Las Exégesis Árabes:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
Ewe Muhammad! Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukuchukia.
Las Exégesis Árabes:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
Na matokeo ya mambo yako, mwisho wake, yatakuwa bora kuliko mwanzo wake.
Las Exégesis Árabes:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
Na ninaapa kuwa bila ya shaka hapo Mola wako Mlezi atakupa kheri za duniani na Akhera hata utaridhia.
Las Exégesis Árabes:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
Kwani hakukukuta wewe yatima unahitaji wa kukutunza naye akakupa makaazi ya kukuhifadhi kwa mwenye kukuangalia vyema kwa mambo yako?
Las Exégesis Árabes:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
Na akakuona umebabaika hukukinaika na itikadi zilizo kuzunguka, naye akakuongoa kwenye Njia ya Haki?
Las Exégesis Árabes:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
Akakukuta fakiri wa mali naye akakutajirisha kwa kukupa riziki?
Las Exégesis Árabes:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimwonee!
Ikiwa hii ndiyo hali yetu nawe, basi yatima usimdhili,
Las Exégesis Árabes:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
Na mwenye kuomba au kuuliza usimjibu kwa ukavu,
Las Exégesis Árabes:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
Na ama neema za Mola wako Mlezi zitangaze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa ndio kudhihirisha neema.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Capítulo: Sura Ad-Dhuhaa
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar