د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - علی محسن البرواني * - د ژباړو فهرست (لړلیک)

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

د معناګانو ژباړه سورت: الضحى   آیت:

Surat Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Naapa kwa mchana!
Naapa kwa wakati wa kupanda juu jua, na ni wakati wa uchangamfu na kazi!
عربي تفسیرونه:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapo tanda!
Na naapa kwa usiku unapo tulia na ukatanda kote kiza chake!
عربي تفسیرونه:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
Ewe Muhammad! Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukuchukia.
عربي تفسیرونه:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
Na matokeo ya mambo yako, mwisho wake, yatakuwa bora kuliko mwanzo wake.
عربي تفسیرونه:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
Na ninaapa kuwa bila ya shaka hapo Mola wako Mlezi atakupa kheri za duniani na Akhera hata utaridhia.
عربي تفسیرونه:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
Kwani hakukukuta wewe yatima unahitaji wa kukutunza naye akakupa makaazi ya kukuhifadhi kwa mwenye kukuangalia vyema kwa mambo yako?
عربي تفسیرونه:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
Na akakuona umebabaika hukukinaika na itikadi zilizo kuzunguka, naye akakuongoa kwenye Njia ya Haki?
عربي تفسیرونه:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
Akakukuta fakiri wa mali naye akakutajirisha kwa kukupa riziki?
عربي تفسیرونه:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimwonee!
Ikiwa hii ndiyo hali yetu nawe, basi yatima usimdhili,
عربي تفسیرونه:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
Na mwenye kuomba au kuuliza usimjibu kwa ukavu,
عربي تفسیرونه:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
Na ama neema za Mola wako Mlezi zitangaze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa ndio kudhihirisha neema.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه سورت: الضحى
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - علی محسن البرواني - د ژباړو فهرست (لړلیک)

سواحلې ژبې ته د قرآن کریم د معناګانو ژباړه، علی محسن البرواني ژباړلې ده

بندول