Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Sura: Sura et-Tekvir   Ajet:

Surat At-Takwir

إِذَا ٱلشَّمۡسُ كُوِّرَتۡ
Pindi jua litakapokunjwa, na mwangaza wake ukaondoka.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتۡ
Na pindi nyota zitakapopuputika na nuru yake ikafutika.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ سُيِّرَتۡ
Na pindi majabali yatakapoondoshawa kwenye uso wa ardhi yakawa ni vumbi linaloenea.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلۡعِشَارُ عُطِّلَتۡ
Na pindi ngamia wenye mimba watakapoachwa na kupuuzwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلۡوُحُوشُ حُشِرَتۡ
Na pindi wanyama mwitu watakapokusanywa na kutangamanishwa, ili Mwenyezi Mungu Awape nafasi ya kulipizana wao kwa wao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ سُجِّرَتۡ
Na pindi bahari zitakapowashwa moto zikawa ni moto unaowaka.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتۡ
Na pindi nafsi zitakapokutanishwa na mfano wake na sampuli yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلۡمَوۡءُۥدَةُ سُئِلَتۡ
Na pindi mtoto wa kike aliyezikwa akiwa hai atakapoulizwa, Siku ya Kiyama, suala la kumbembeleza na kumkejeli aliyemzika:
Tefsiri na arapskom jeziku:
بِأَيِّ ذَنۢبٖ قُتِلَتۡ
ni kwa dhambi gani ilikuwa kuzikwa kwake?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ
Na pindi kurasa za matendo zitakapoonyeshwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتۡ
Na pindi mbingu zitakapong’olewa na kuondoshwa zilipokuwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ
Na pindi Moto utakapowashwa na ukawaka.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ
Na pindi Pepo , Nyumba ya Neema, itakaposongezewa watu wake wachamungu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ
Litakapotokea hilo, itayakinisha kila nafsi na kujua kile ilichokitanguliza cha kheri au shari.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ
Anaapa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa nyota zinazofichika nuru yake mchana,
Tefsiri na arapskom jeziku:
ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ
zinazotembea na zinazoghibu katika anga zake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ
Na Anaapa kwa usiku unapojitokeza na giza lake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Na kwa asubuhi unapojitokeza mwangaza wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Hakika Qur’ani ni ujumbe wa mjumbe mtukufu , naye ni Jibrili, amani imshukike.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ
Mwenye nguvu katika kuyapitisha yale anayoamrishwa. Mwenye cheo cha juu kwa Mwenyezi Mungu. Anayesikilizwa na Malaika.
Tefsiri na arapskom jeziku:
مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ
Anayeaminiwa juu ya Wahyi anaoteremka nao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ
Hakuwa Muhammad mnayemjua ni mwendawazimu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ
Na kwa hakika Muhammad alimuona Jibrili anayemjia na utume katika pambizo kubwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ
Wala yeye hafanyi ubakhili katika kufikisha Wahyi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ
Wala haikuwa hii Qur’ani ni neno la Shetani aliyefukuzwa na kutolewa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu. Lakini Qur’ani hii ni maneno ya Mwenyezi Mungu na ni Wahyi wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ
Akili zenu zawapeleka wapi katika kukanusha baada ya hoja hizi zilizo wazi na zenye nguvu?
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Hayakuwa haya isipokuwa ni mawaidha kutoka kwa Mwenyezi Mungu yanapewa watu wote.
Tefsiri na arapskom jeziku:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ
Kwa atakaye, kati yenu, kulingana juu ya haki na Imani.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala nyinyi hamtotaka isipokuwa kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: Sura et-Tekvir
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Zatvaranje