ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی سوره: سوره شرح   آیه:

Surat Ash-Sharh

أَلَمۡ نَشۡرَحۡ لَكَ صَدۡرَكَ
Kwani Hatukukunjulia, ewe Mtume, kifua chako kwa sheria za Dini, kulingania watu kwa Mwenyezi Mungu na kujipamba kwa tabia nzuri,
تفسیرهای عربی:
وَوَضَعۡنَا عَنكَ وِزۡرَكَ
Tukakuondolea mazito yako yaliyoemea mgongo wako
تفسیرهای عربی:
ٱلَّذِيٓ أَنقَضَ ظَهۡرَكَ
na Tukakuweka, kwa matukufu Tuliyokuneemesha,
تفسیرهای عربی:
وَرَفَعۡنَا لَكَ ذِكۡرَكَ
kwenye cheo cha juu?
تفسیرهای عربی:
فَإِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرًا
Usirudi nyuma katika kueneza ujumbe uliotumwa nao kwa makero ya maadui zako. Kwani kwenye dhiki kuna faraji.
تفسیرهای عربی:
إِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرٗا
Hakika kwenye dhiki kuna faraji.
تفسیرهای عربی:
فَإِذَا فَرَغۡتَ فَٱنصَبۡ
Basi utakapomaliza mambo ya kidunia na shughuli zake jipinde kwa kufanya ibada.
تفسیرهای عربی:
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرۡغَب
Na kwa Mola wako Peke Yake weka matumaini yako.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی سوره: سوره شرح
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی. ترجمهٔ دکتر عبدالله محمد ابوبکر و شیخ ناصر خمیس.

بستن