क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस * - अनुवादों की सूची


अर्थों का अनुवाद सूरा: सूरा अल्-हु-म-ज़ह   आयत:

Surat Al-Humazah

وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ
Shari na maangamivu yatampata kila mwenye kusengenya watu na kuwatukana.
अरबी तफ़सीरें:
ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ
Ambaye hamu yake ni kukusanya mali na kuyahesabu.
अरबी तफ़सीरें:
يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ
Akidhani kuwa mali yake ambayo ameyakusanya yatampa dhamana ya kuishi milele duniani na kuhepa kuhesabiwa.
अरबी तफ़सीरें:
كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ
Anavyodhania sivyo. Atatiwa ndani ya Moto ambao huvunjavunja kila kinachotiwa.
अरबी तफ़सीरें:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ
Lipi lililokujulisha, ewe Mtume, ni upi huo Moto unaovunjavunja?
अरबी तफ़सीरें:
نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ
Huo ni Moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa.
अरबी तफ़सीरें:
ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ
Ambao kwa ukali wake hupenyeza miilini ukafikia kwenye nyoyo.
अरबी तफ़सीरें:
إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ
Moto huo umefungiwa juu yao wakiwa wametiwa minyororo
अरबी तफ़सीरें:
فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ
na pingu ndefu ili wasitoke.
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद सूरा: सूरा अल्-हु-म-ज़ह
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस - अनुवादों की सूची

पवित्र क़ुरआन के अर्थों का सवाहिली अनुवाद, अनुवादक : डॉ. अब्दुल्लाह मुहम्मद अबू बक्र तथा शैख़ नासिर ख़मीस

बंद करें