Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis * - Indice Traduzioni


Traduzione dei significati Sura: Al-Burûj   Versetto:

Surat Al-Buruj

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡبُرُوجِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu zenye njia za kupitia jua na mwezi.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡمَوۡعُودِ
Na kwa Siku ya Kiyama ambayo Amewaahidi viumbe kuwa Atawakusanya.
Esegesi in lingua araba:
وَشَاهِدٖ وَمَشۡهُودٖ
Na kwa shahidi, mwenye kutoa ushahidi, na mwenye kutolewa ushahidi juu yake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Anachokitaka. Lakini kiumbe hafai kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Esegesi in lingua araba:
قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ
Wamelaaniwa waliofukua chini ya ardhi shimo kubwa ili kuwatesa Waumini.
Esegesi in lingua araba:
ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ
Wakawasha moto mkubwa wenye kuni nyingi.
Esegesi in lingua araba:
إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ
Wakawa wamekaa kwenye kingo za shimo hilo.
Esegesi in lingua araba:
وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ
Wakishuhudia vitendo vya mateso na adhabu wanavyowafanyia Waumini.
Esegesi in lingua araba:
وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ
Na hawakuwatesa mateso hayo isipokuwa wenye kuteswa walikuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu Mshindi Asiyeshindwa, Mhimidiwa wa maneno Yake vitendo Vyake na sifa Zake.
Esegesi in lingua araba:
ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ
Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi Ambaye, kutakasika na sifa za upungufu ni kwake, Anashuhudia kila kitu, hakuna kinachofichika kwake.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ
Hakika, wale waliowachoma kwa moto Waumini, wa kike na wa kiume, ili kuwazuia watu na dini ya Mwenyezi Mungu, kisha wasitubie, watapata, Siku ya Akhera, adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu kali yenye kuchoma.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya amali njema, watapata Pepo ambayo chini ya majumba yake ya kifahari yapita mito. Huko ni kufaulu kukubwa.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
Hakika malipizo ya Mola wako kwa maadui Zake na mateso Yake juu yao ni mazito.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ
Ndiye Yeye Mwenye kuanzisha kuumba na kisha kurudisha.
Esegesi in lingua araba:
وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ
Ndiye Yeye Mwingi wa kusamehe kwa wenye kutubia, Mwingi wa mapenzi kwa wanaoikurubisha kwake.
Esegesi in lingua araba:
ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ
Mwenye Arshi tukufu.
Esegesi in lingua araba:
فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ
Mfanya Alitakalo: hakuna kitu Anachotaka kiwe kisiwe.
Esegesi in lingua araba:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ
Je, ewe Mtume, imekufikia habari ya makundi yaliyokufuru na kukanusha Mitume walioletwa, ya
Esegesi in lingua araba:
فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ
Firauni na Thamūd, misiba na adhabu iliyowashukia? Hawakuzingatia kwa habari hiyo.
Esegesi in lingua araba:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ
Bali waliokufuru waendelea kukanusha kwao, kama walivyokuwa waliokuja kabla yao.
Esegesi in lingua araba:
وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ
Na Mwenyezi Mungu Amewazunguka kwa Ujuzi na Uweza Wake, hakuna chenye kufichika Kwake kuhusu wao na vitendo vyao. Hii Qu’ani siyo kama wanavyodai wenye kukanusha katika washirikina kuwa ni mashairi na uchawi ndipo wakaikanusha.
Esegesi in lingua araba:
بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ
Bali hii ni Qur’ani kubwa iliyo tukufu,
Esegesi in lingua araba:
فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ
iliyomo kwenye Ubao Uliohifadhiwa, haufikiwi na kubadilishwa wala kupotoshwa.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Sura: Al-Burûj
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Abdullah Mohammed ِAbu Bakr e Shaikh Nasser Khamis

Chiudi