32 : 68

عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ

Tunatarajia kwa Mola wetu kuwa Atatupa kilicho bora zaidi kuliko shamba letu, kwa kuwa tumetubia na tumekubali makosa yetu. Sisi tuna matumaini mema kwa Mola wetu, tunatarajia msamaha na tunaomba kheri. Mfano wa mateso hayo tuliyowatesa nayo wenye shamba, ndivyo yanavyokuwa mateso yetu duniani kwa kila anayeenda kinyume na amri ya Allah Mtukufu, na akazifanyia uchoyo neema za Allah Mtukufu Alizompa, kwa kutotekeleza haki ya Allah Mtukufu katika neema hizo. info
التفاسير: |
prev

Al-Qalam

next
:
0:00 0:00