Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis * - Vertimų turinys


Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Ad-Duchaa   Aja (Korano eilutė):

Surat Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa dhuha, na uliokusudiwa ni wakati wa mchana mzima.
Tafsyrai arabų kalba:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku utuliapo na viumbe na likashadidi giza lake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Atakacho katika viumbe vyake. Ama kiumbe, hafai kuapa kwa asiyekuwa Muumba wake. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Tafsyrai arabų kalba:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Hakukuwacha Mola wako, ewe Mtume, wala Hakukuchukia kwa kuchelewesha kukuteremshiaWahyi.
Tafsyrai arabų kalba:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na Nyumba ya Akhera ni bora kwako kuliko nyumba ya ulimwengu.
Tafsyrai arabų kalba:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Atakupa Mola wako, ewe Mtume, neema ya kila sampuli uridhike.
Tafsyrai arabų kalba:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani Hakukupata, kabla ya hapo, kuwa ni yatima Akakukusanya na kukutunza.
Tafsyrai arabų kalba:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na Akakupata hujui Kitabu wala Imani, Akakufundisha yale amabayo ulikuwa huyajui na akakuafikia kufanya amali bora?
Tafsyrai arabų kalba:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Na Akakupata masikini, Akakuletea riziki yako na Akakutajirisha kwa kutosheka na kusubiri?
Tafsyrai arabų kalba:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimtende ubaya.
Tafsyrai arabų kalba:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na muombaji usimkaripie, bali mlishe na umtimizie haja yake.
Tafsyrai arabų kalba:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na ama neema ya Mola wako Aliyokuneemesha nayo izungumze.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Ad-Duchaa
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Dr. Abdullah Muchammed Abu Bakr ir šeichas Naser Khamis.

Uždaryti