Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis * - Índice de tradução


Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Ala   Versículo:

Surat Al-A'la

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى
Takasa Jina la Mola wako Aliyetukuka na kuepukana na mshirika na kila sifa pungufu kwa namna inayonasibiana na utukufu Wake na utakatifu Wake.
Os Tafssir em língua árabe:
ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Aliyeumba viumbe Akalitengeneza umbo lao na kulifanya zuri.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Na Aliyekadiria kila kitu na kukipeleka njia inayonasibiana nacho.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ
Na Aliyeotesha nyasi mbiti zenye rangi ya kijani,
Os Tafssir em língua árabe:
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ
Akazifanya baadaye kuwa kavu zilizobadilika rangi.
Os Tafssir em língua árabe:
سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Tutakusomea, ewe Mtume, hii Qur’ani kisomo ambacho hutakisahau.
Os Tafssir em língua árabe:
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ
Isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Ataka usahau kwa hekima na maslahi anayoyajua Yeye. Kwani Yeye ni Mjuzi wa yaliyo wazi na yaliyofichika, ya maneno na ya vitendo.
Os Tafssir em língua árabe:
وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutakufanyia mapesi mambo yako yote; miongoni mwayo ni kukusahilishia kubeba majukumu ya utume na kuifanya nyepesi Dini uliyokuja nayo.
Os Tafssir em língua árabe:
فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ
Basi wawaidhie kaumu zako, ewe Mtume, kwa namna tulivyokutayarishia ufanye kwenye wahyi ulioletewa, uwaongoze njia yenye kheri na wao na uwahusu kwa mawaidha yako wale wanaotarajiwa kuwaidhika nayo. Wala usijisumbue kuwashauri wale ambao mawidha hayawaathiri isipokuwa kuwatia ujeuri na kuwafanya wayakimbie.
Os Tafssir em língua árabe:
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ
Atanufaika kwa mawaidha anayemcha Mola wke,
Os Tafssir em língua árabe:
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى
na atajiepusha na mawaidha aliye mbaya asiyemuogopa Mola wake
Os Tafssir em língua árabe:
ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
atakayeingia kwenye Moto wa Jahanamu akiadhibika kwa ukali wake.
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ
Kisha hatakuwa ni mwenye kufa akapumzika wala ni mwenye kuishi akanufaika.
Os Tafssir em língua árabe:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake na tabia mbovu,
Os Tafssir em língua árabe:
وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
na akamtaja Mwenyezi Mungu, akampwekesha, akamuomba, akafanya vitendo vya kumridhisha na akasimamisha Swala kwa nyakati zake kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kufuata sheria Aliyoiweka.
Os Tafssir em língua árabe:
بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Hakika yenu, nyinyi watu, mnafadhilisha pambo la maisha ya kilimwengu juu ya starehe za Akhera.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ
Na hakika ya mambo ni kuwa nyumba ya Akhera na starehe zake ni bora zaidi kuliko ulimwngu na ni yenye kusalia zaidi.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ
Haya mlioosimuliwa ndani ya Sura hii ni miongoni mwa yaliyotajwa kimaana katika Kurasa zilizotangulia kuteremshwa kabla ya Qur’ani.
Os Tafssir em língua árabe:
صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Nazo ni Kurasa za Ibrāhīm na Mūsā, amani ziwashukie.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Ala
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão em suaíli pelo Dr. Abdalla Mohamed Abubakar e Nassor Khamis

Fechar