قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ تکویر   آیت:

Surat At-Takwir

إِذَا ٱلشَّمۡسُ كُوِّرَتۡ
Pindi jua litakapokunjwa, na mwangaza wake ukaondoka.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتۡ
Na pindi nyota zitakapopuputika na nuru yake ikafutika.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ سُيِّرَتۡ
Na pindi majabali yatakapoondoshawa kwenye uso wa ardhi yakawa ni vumbi linaloenea.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلۡعِشَارُ عُطِّلَتۡ
Na pindi ngamia wenye mimba watakapoachwa na kupuuzwa.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلۡوُحُوشُ حُشِرَتۡ
Na pindi wanyama mwitu watakapokusanywa na kutangamanishwa, ili Mwenyezi Mungu Awape nafasi ya kulipizana wao kwa wao.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ سُجِّرَتۡ
Na pindi bahari zitakapowashwa moto zikawa ni moto unaowaka.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتۡ
Na pindi nafsi zitakapokutanishwa na mfano wake na sampuli yake.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلۡمَوۡءُۥدَةُ سُئِلَتۡ
Na pindi mtoto wa kike aliyezikwa akiwa hai atakapoulizwa, Siku ya Kiyama, suala la kumbembeleza na kumkejeli aliyemzika:
عربی تفاسیر:
بِأَيِّ ذَنۢبٖ قُتِلَتۡ
ni kwa dhambi gani ilikuwa kuzikwa kwake?
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ
Na pindi kurasa za matendo zitakapoonyeshwa.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتۡ
Na pindi mbingu zitakapong’olewa na kuondoshwa zilipokuwa.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ
Na pindi Moto utakapowashwa na ukawaka.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ
Na pindi Pepo , Nyumba ya Neema, itakaposongezewa watu wake wachamungu.
عربی تفاسیر:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ
Litakapotokea hilo, itayakinisha kila nafsi na kujua kile ilichokitanguliza cha kheri au shari.
عربی تفاسیر:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ
Anaapa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa nyota zinazofichika nuru yake mchana,
عربی تفاسیر:
ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ
zinazotembea na zinazoghibu katika anga zake.
عربی تفاسیر:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ
Na Anaapa kwa usiku unapojitokeza na giza lake.
عربی تفاسیر:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Na kwa asubuhi unapojitokeza mwangaza wake.
عربی تفاسیر:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Hakika Qur’ani ni ujumbe wa mjumbe mtukufu , naye ni Jibrili, amani imshukike.
عربی تفاسیر:
ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ
Mwenye nguvu katika kuyapitisha yale anayoamrishwa. Mwenye cheo cha juu kwa Mwenyezi Mungu. Anayesikilizwa na Malaika.
عربی تفاسیر:
مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ
Anayeaminiwa juu ya Wahyi anaoteremka nao.
عربی تفاسیر:
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ
Hakuwa Muhammad mnayemjua ni mwendawazimu.
عربی تفاسیر:
وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ
Na kwa hakika Muhammad alimuona Jibrili anayemjia na utume katika pambizo kubwa.
عربی تفاسیر:
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ
Wala yeye hafanyi ubakhili katika kufikisha Wahyi.
عربی تفاسیر:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ
Wala haikuwa hii Qur’ani ni neno la Shetani aliyefukuzwa na kutolewa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu. Lakini Qur’ani hii ni maneno ya Mwenyezi Mungu na ni Wahyi wake.
عربی تفاسیر:
فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ
Akili zenu zawapeleka wapi katika kukanusha baada ya hoja hizi zilizo wazi na zenye nguvu?
عربی تفاسیر:
إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Hayakuwa haya isipokuwa ni mawaidha kutoka kwa Mwenyezi Mungu yanapewa watu wote.
عربی تفاسیر:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ
Kwa atakaye, kati yenu, kulingana juu ya haki na Imani.
عربی تفاسیر:
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala nyinyi hamtotaka isipokuwa kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ تکویر
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے کیا ہے۔

بند کریں