《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 阿拜萨   段:

Surat Abasa

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Yalidhihiri mabadiliko na mkunjiko katika uso wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
阿拉伯语经注:
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
na akapa nyongo kwa sababu ya kwamba Abdallah bin Ummi Maktum alimjilia akitaka aelekezwe. Na alikuwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ameshughulika kuwalingania miamba wa Kikureshi katika Uislamu.
阿拉伯语经注:
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Ni kitu gani kinakufanya wewe ujue uhakika wa jambo lake? Kwani huenda ikawa, kwa kuuliza kwake, nafsi yake itatakasika na kusafika.
阿拉伯语经注:
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au pengine apate mazingatio zaidi na kutishika.
阿拉伯语经注:
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Basi yule alijyejitosheleza na kutouhitajia uongozi wako,
阿拉伯语经注:
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
wewe ndiye unayemjali na wapulikiza maneno yake.
阿拉伯语经注:
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na ni kitu gani kinachokupa jukumu kwako iwapo hakusafika na ukafiri wake?
阿拉伯语经注:
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama yule ambaye amekuwa na pupa la kukutana na wewe,
阿拉伯语经注:
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
na huku anamuogopa Mwenyezi Mungu asiwe na kasoro katika kupata uongofu,
阿拉伯语经注:
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
wewe unampuuza. Ilivyotakikana ufanye si kama ulivyofanya, ewe Mtume.
阿拉伯语经注:
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Hakika Sura hii ni mawaidha kwako na kwa kila anayetaka kuwaidhika.
阿拉伯语经注:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi atakaye atamkumbuka Mwenyezi Mungu na kumtaja na atafuata Wahyi Wake.
阿拉伯语经注:
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Wahyi huu, nao ni Qur’ani, uko katika kurasa zilizotukuzwa,
阿拉伯语经注:
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
zenye kuheshimiwa, zenye cheo cha juu,
阿拉伯语经注:
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
zilizosafishwa na uchafu, uongezaji na upunguzaji.
阿拉伯语经注:
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Zilizoko mikononi mwa Malaika waandishi, mabalozi kati ya Mwenyezi Mungu na viumbe Wake, wenye maumbile mema, tabia zao ni nzuri na njema na pia matendo yao.
阿拉伯语经注:
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Amelaaniwa mtu kafiri na ataadhibiwa. Ni uovu ulioje wa ukafiri wake kwa Mola wake!
阿拉伯语经注:
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwani hajui ni kwa kitu gani Mwenyezi Mungu Alimuumba kwacho mwanzo wake?
阿拉伯语经注:
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Mwenyezi Mungu Alimuumba kwa maji machache, nayo ni manii. Akayakadiria miongo yake.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha Akambainishia njia ya kheri na ya shari.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha humkosesha uhai, na Amemuekea mahali pa kuzikiwa.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha Akitaka Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na sifa mbaya, Atamhuisha na kumfufua baada ya kifo chake, kwa ajili ya kuhesabiwa na kulipwa.
阿拉伯语经注:
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
Mambo siyo kama yale anayoyasema kafiri na anayoyafanya. Bado hajatakeleza Aliyomuamrisha kwayo Mwenyezi Mungu katika kuamini na kutenda wema kwa kumtii.
阿拉伯语经注:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Na azingatie binadamu, vipi Mwenyezi Mungu Amekiumba chakula chake ambacho ndicho kinachoendeleza maisha yake?
阿拉伯语经注:
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Aone kwamba Sisi Tumeyamimina maji ya mvua juu ya ardhi kwa wingi.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Kisha Tumeipasua ardhi kwa Tulivyo vitoa kutoka humo miongoni mwa mimea tofauti.
阿拉伯语经注:
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Tukaotesha humo nafaka
阿拉伯语经注:
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
na zabibu, na nyasi za wanyama.Na mizaituni na mitende.
阿拉伯语经注:
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mabustani yenye miti mikubwa.
阿拉伯语经注:
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na matunda
阿拉伯语经注:
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
na ndisha.
阿拉伯语经注:
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Mnajistareheshea kwazo, nyinyi na wanyama wenu.
阿拉伯语经注:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Utakapokuja Ukelele wa Siku ya Kiyama, ambao utayatia uziwi, kwa kitisho chake, masikizi.
阿拉伯语经注:
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku mtu atakapomkimbia, kwa kitisho cha Siku Hiyo, nduguye
阿拉伯语经注:
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
na babake na mamake na
阿拉伯语经注:
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
mkewe na wanawe.
阿拉伯语经注:
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mmoja Siku Hiyo, atakuwa na jambo litakalomzuia asishughulike na mwingine.
阿拉伯语经注:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Nyuso za wenye neema, Siku Hiyo, zitakuwa ni zenye kung’ara,
阿拉伯语经注:
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
zenye furaha na nderemo.
阿拉伯语经注:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso za watu wa Motoni zitakuwa na giza,
阿拉伯语经注:
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
nyeusi, zafinikwa na unyonge.
阿拉伯语经注:
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao wenye kusifika na sifa hiyo ndiwo wale waliozikufuru neema za Mwenyezi Mungu na wakazikanusha aya zake na wakayakeuka Aliyoyaharamisha kwa kutenda maovu na kukiuka mipaka.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 阿拜萨
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭