ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್ * - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ


ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಸೂರ ಅಬಸ್   ಶ್ಲೋಕ:

Surat Abasa

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Yalidhihiri mabadiliko na mkunjiko katika uso wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
na akapa nyongo kwa sababu ya kwamba Abdallah bin Ummi Maktum alimjilia akitaka aelekezwe. Na alikuwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ameshughulika kuwalingania miamba wa Kikureshi katika Uislamu.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Ni kitu gani kinakufanya wewe ujue uhakika wa jambo lake? Kwani huenda ikawa, kwa kuuliza kwake, nafsi yake itatakasika na kusafika.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au pengine apate mazingatio zaidi na kutishika.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Basi yule alijyejitosheleza na kutouhitajia uongozi wako,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
wewe ndiye unayemjali na wapulikiza maneno yake.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na ni kitu gani kinachokupa jukumu kwako iwapo hakusafika na ukafiri wake?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama yule ambaye amekuwa na pupa la kukutana na wewe,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
na huku anamuogopa Mwenyezi Mungu asiwe na kasoro katika kupata uongofu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
wewe unampuuza. Ilivyotakikana ufanye si kama ulivyofanya, ewe Mtume.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Hakika Sura hii ni mawaidha kwako na kwa kila anayetaka kuwaidhika.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi atakaye atamkumbuka Mwenyezi Mungu na kumtaja na atafuata Wahyi Wake.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Wahyi huu, nao ni Qur’ani, uko katika kurasa zilizotukuzwa,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
zenye kuheshimiwa, zenye cheo cha juu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
zilizosafishwa na uchafu, uongezaji na upunguzaji.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Zilizoko mikononi mwa Malaika waandishi, mabalozi kati ya Mwenyezi Mungu na viumbe Wake, wenye maumbile mema, tabia zao ni nzuri na njema na pia matendo yao.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Amelaaniwa mtu kafiri na ataadhibiwa. Ni uovu ulioje wa ukafiri wake kwa Mola wake!
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwani hajui ni kwa kitu gani Mwenyezi Mungu Alimuumba kwacho mwanzo wake?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Mwenyezi Mungu Alimuumba kwa maji machache, nayo ni manii. Akayakadiria miongo yake.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha Akambainishia njia ya kheri na ya shari.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha humkosesha uhai, na Amemuekea mahali pa kuzikiwa.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha Akitaka Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na sifa mbaya, Atamhuisha na kumfufua baada ya kifo chake, kwa ajili ya kuhesabiwa na kulipwa.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
Mambo siyo kama yale anayoyasema kafiri na anayoyafanya. Bado hajatakeleza Aliyomuamrisha kwayo Mwenyezi Mungu katika kuamini na kutenda wema kwa kumtii.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Na azingatie binadamu, vipi Mwenyezi Mungu Amekiumba chakula chake ambacho ndicho kinachoendeleza maisha yake?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Aone kwamba Sisi Tumeyamimina maji ya mvua juu ya ardhi kwa wingi.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Kisha Tumeipasua ardhi kwa Tulivyo vitoa kutoka humo miongoni mwa mimea tofauti.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Tukaotesha humo nafaka
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
na zabibu, na nyasi za wanyama.Na mizaituni na mitende.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mabustani yenye miti mikubwa.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na matunda
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
na ndisha.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Mnajistareheshea kwazo, nyinyi na wanyama wenu.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Utakapokuja Ukelele wa Siku ya Kiyama, ambao utayatia uziwi, kwa kitisho chake, masikizi.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku mtu atakapomkimbia, kwa kitisho cha Siku Hiyo, nduguye
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
na babake na mamake na
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
mkewe na wanawe.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mmoja Siku Hiyo, atakuwa na jambo litakalomzuia asishughulike na mwingine.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Nyuso za wenye neema, Siku Hiyo, zitakuwa ni zenye kung’ara,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
zenye furaha na nderemo.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso za watu wa Motoni zitakuwa na giza,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
nyeusi, zafinikwa na unyonge.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao wenye kusifika na sifa hiyo ndiwo wale waliozikufuru neema za Mwenyezi Mungu na wakazikanusha aya zake na wakayakeuka Aliyoyaharamisha kwa kutenda maovu na kukiuka mipaka.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
 
ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಸೂರ ಅಬಸ್
ಅಧ್ಯಾಯಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ ಪುಟ ಸಂಖ್ಯೆ
 
ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್ - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ

ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಡಾ. ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಅಬೂಬಕರ್ ಮತ್ತು ಶೈಖ್ ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್

ಮುಚ್ಚಿ