Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Simoore: Simoore feƴ-naange   Aaya:

Surat Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa dhuha, na uliokusudiwa ni wakati wa mchana mzima.
Faccirooji aarabeeji:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku utuliapo na viumbe na likashadidi giza lake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Atakacho katika viumbe vyake. Ama kiumbe, hafai kuapa kwa asiyekuwa Muumba wake. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Faccirooji aarabeeji:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Hakukuwacha Mola wako, ewe Mtume, wala Hakukuchukia kwa kuchelewesha kukuteremshiaWahyi.
Faccirooji aarabeeji:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na Nyumba ya Akhera ni bora kwako kuliko nyumba ya ulimwengu.
Faccirooji aarabeeji:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Atakupa Mola wako, ewe Mtume, neema ya kila sampuli uridhike.
Faccirooji aarabeeji:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani Hakukupata, kabla ya hapo, kuwa ni yatima Akakukusanya na kukutunza.
Faccirooji aarabeeji:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na Akakupata hujui Kitabu wala Imani, Akakufundisha yale amabayo ulikuwa huyajui na akakuafikia kufanya amali bora?
Faccirooji aarabeeji:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Na Akakupata masikini, Akakuletea riziki yako na Akakutajirisha kwa kutosheka na kusubiri?
Faccirooji aarabeeji:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimtende ubaya.
Faccirooji aarabeeji:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na muombaji usimkaripie, bali mlishe na umtimizie haja yake.
Faccirooji aarabeeji:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na ama neema ya Mola wako Aliyokuneemesha nayo izungumze.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simoore feƴ-naange
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude