કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ * - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા


શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ લૈલ   આયત:

Surat Al-Lail

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa usiku unapoifinika ardhi na vilivyoko juu yake kwa giza lake.
અરબી તફસીરો:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na kwa mchana unapofunuka mwangaza wake kutoka kwenye giza la usiku.
અરબી તફસીરો:
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Na kwa kuumba mbea mbili: ya kiume na ya kike,
અરબી તફસીરો:
إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ
Kuwa vitendo vyenu vinatofautiana: kuna wenye kufanyia dunia na wenye kufanyia Akhera.
અરબી તફસીરો:
فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa kwenye mali yake, akamcha Mwenyezi Mungu katika huko kutoa,
અરબી તફસીરો:
وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
akaamini «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na Imani hiyo na akaamini malipo yanayofungamana nayo,
અરબી તફસીરો:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutamuongoza na kumuafikia njia za kheri na wema na kumsahilishia mambo yake.
અરબી તફસીરો:
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ
Na ama mwenye kuyafanyia ubakhili mali yake, asiwe na haja ya malipo ya Mola wake,
અરબી તફસીરો:
وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
akakanusha neno la «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na neno hilo na akakanusha malipo yanayofungamana nalo,
અરબી તફસીરો:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡعُسۡرَىٰ
Tutamnyoshea njia za mateso.
અરબી તફસીરો:
وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Wala hayatamfaa yeye mali yake aliyoyafanyia ubakhili atakapotumbukia Motoni.
અરબી તફસીરો:
إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ
Ni juu Yetu, kwa fadhila Zetu na busara Yetu, kueleza njia ya uongofu yenye kufikisha kwa Mwenyezi Mungu na ya upotevu.
અરબી તફસીરો:
وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ
Na Sisi Tuna mamlaka ya maisha ya Akhera na maisha ya ulimwenguni.
અરબી તફસીરો:
فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ
Ndipo nikawaonya , enyi watu, na kuwatisha moto wenye kuwaka, nao ni moto wa Jahanamu.
અરબી તફસીરો:
لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى
Hataingia Moto huo isipokuwa aliyekuwa mbaya sana. Mwenye kumkanusha Nabii Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
અરબી તફસીરો:
ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
na akakataa kumwamini na kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
અરબી તફસીરો:
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى
Na ataepushwa nao mchaji Mwenyezi Mungu sana.
અરબી તફસીરો:
ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Ambaye hutoa mali yake kwa kutaka nyongeza za kheri
અરબી તફસીરો:
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ
kutoa Kwake si kwa kulipa zema alizofanyiwa na mtu.
અરબી તફસીરો:
إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Lakini anatoa kwa kutaka uso wa Mola wake na radhi zake. Basi Mwenyezi Mungu atampa,
અરબી તફસીરો:
وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ
huko Peponi, malipo ya kumridhisha.
અરબી તફસીરો:
 
શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ લૈલ
સૂરહ માટે અનુક્રમણિકા પેજ નંબર
 
કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

સ્વાહિલી ભાષામાં કુરઆન મજીદનું ભાષાતર, ભાષાતર કરનારનું નામ અદ્ દૂકતુર અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અબૂ બકર અને શેખ નાસીર ખમીસ

બંધ કરો