Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Layl   Ayah:

Surat Al-Lail

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa usiku unapoifinika ardhi na vilivyoko juu yake kwa giza lake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na kwa mchana unapofunuka mwangaza wake kutoka kwenye giza la usiku.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Na kwa kuumba mbea mbili: ya kiume na ya kike,
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ
Kuwa vitendo vyenu vinatofautiana: kuna wenye kufanyia dunia na wenye kufanyia Akhera.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa kwenye mali yake, akamcha Mwenyezi Mungu katika huko kutoa,
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
akaamini «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na Imani hiyo na akaamini malipo yanayofungamana nayo,
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutamuongoza na kumuafikia njia za kheri na wema na kumsahilishia mambo yake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ
Na ama mwenye kuyafanyia ubakhili mali yake, asiwe na haja ya malipo ya Mola wake,
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
akakanusha neno la «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na neno hilo na akakanusha malipo yanayofungamana nalo,
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡعُسۡرَىٰ
Tutamnyoshea njia za mateso.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Wala hayatamfaa yeye mali yake aliyoyafanyia ubakhili atakapotumbukia Motoni.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ
Ni juu Yetu, kwa fadhila Zetu na busara Yetu, kueleza njia ya uongofu yenye kufikisha kwa Mwenyezi Mungu na ya upotevu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ
Na Sisi Tuna mamlaka ya maisha ya Akhera na maisha ya ulimwenguni.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ
Ndipo nikawaonya , enyi watu, na kuwatisha moto wenye kuwaka, nao ni moto wa Jahanamu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى
Hataingia Moto huo isipokuwa aliyekuwa mbaya sana. Mwenye kumkanusha Nabii Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
Ang mga Tafsir na Arabe:
ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
na akakataa kumwamini na kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى
Na ataepushwa nao mchaji Mwenyezi Mungu sana.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Ambaye hutoa mali yake kwa kutaka nyongeza za kheri
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ
kutoa Kwake si kwa kulipa zema alizofanyiwa na mtu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Lakini anatoa kwa kutaka uso wa Mola wake na radhi zake. Basi Mwenyezi Mungu atampa,
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ
huko Peponi, malipo ya kumridhisha.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Layl
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis - Indise ng mga Salin

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an sa Wikang Swahili. Isinalin ito nina Doktor Abdullah Muhammad Abu Bakr at Shaykh Nasir Khamis. Inilathala ito ng King Fahd Glorious Quran Printing Complex sa Madinah Munawwarah, imprenta ng taong 1435 H.

Isara