Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da yaren Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Sura: Suratu Al'nazi'at   Aya:

Surat An-Nazi'at

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Malaika ambao huzing’oa roho za makafiri mng’oo mkali.
Tafsiran larabci:
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا
Na kwa Malaika ambao huzitukua roho za Waumini kwa uchangamfu na upole.
Tafsiran larabci:
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا
Na kwa Malaika wanaoogelea katika kushuka kwao kutoka mbinguni na kupaa kwao kwenda mbinguni.
Tafsiran larabci:
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا
Na kwa Mlaika ambao wanakimbilia kutekeleza amri za Mwenyezi Mungu.
Tafsiran larabci:
فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا
Na kwa Malaika wanaopitisha amri za Mola wao katika mambo ya ulimwengu waliowakilishwa kuyafanya na kuyasimamia, - Wala haifai kwa kiumbe kukiapia chochote kile, bali yapasa kiapo chake kiwe ni kwa jina la Mola wake Muumba au sifa Zake. Na lau ataapa kwa asiye Muumba wake, basi huyo amekuwa mshirikina - Watafufuliwa viumbe bila shaka na watahesabiwa.
Tafsiran larabci:
يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku ambayo ardhi itatetemeka kwa mvuvuo wa kwanza:
Tafsiran larabci:
تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
mvuvio wa kufisha, ukifuatiwa na mvuvio mwingine wa kuhuisha.
Tafsiran larabci:
قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ
Nyoyo za makafiri, Siku hiyo, zitakuwa na papatiko kwa kicho kikubwa.
Tafsiran larabci:
أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ
Macho ya makafiri hao yatakuwa madhalilifu kwa kitisho watakachokiona.
Tafsiran larabci:
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ
Wanasema hawa wakanushao kufufuliwa:
Tafsiran larabci:
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ
«Je, tutarudishwa baada ya kufa kwetu kwenye yale tuliyokuwa nayo katika ardhi? Je, tutarudishwa na hali tushakuwa mifupa iliochakaa?»
Tafsiran larabci:
قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ
Wakasema: «Kurejea kwetu huko kutakuwa kutupu kusikokuwa kweli.’
Tafsiran larabci:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ
Hakika tukio hilo litakuwa kwa mvivio mmoja tu.
Tafsiran larabci:
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Wakitahamaki wao wako hai juu ya ardhi baada ya kuwa walikuwa ndani yake.
Tafsiran larabci:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je imekujilia, ewe Mtume, habari ya Mūsā?
Tafsiran larabci:
إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى
Pindi Mola wake Alipomwita katika bonde lililotakaswa na kubarikiwa, la Ṭuwā. Akamwambia:
Tafsiran larabci:
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
«Enda kwa Firauni. Hakika yeye amekiuka mno katika kuasi.
Tafsiran larabci:
فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Ukamwambie, ‘Je, unapendelea kuitakasa nafsi yako na upungufu na kuipamba na imani?
Tafsiran larabci:
وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ
Na nikuelekeze njia ya kumtii Mola wako, upate kumcha na kumuogopa?’»
Tafsiran larabci:
فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Mūsā alimuonyesha Firauni alama kubwa: fimbo na mkono.
Tafsiran larabci:
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Hapo Firauni alimkanusha Nabii wa Mwenyezi Mungu , naye ni Mtume Mūsā, amani imshukie, na alimuasi Mola wake Aliyetukuka.
Tafsiran larabci:
ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ
Kisha alikengeuka hali ya kuipa mgongo Imani na kufanya bidii katika kumpinga Mūsā.
Tafsiran larabci:
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Hapo aliwakusanya raia wa utawala wake na akawaita kwa
Tafsiran larabci:
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ
kuwaambia,»Mimi ndiye mola wenu ambaye hakuna mola mwengine aliye juu yake.»
Tafsiran larabci:
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ
Hapo Mwenyezi Mungu Alimtesa kwa adhabu ya duniani na ya Akhera.
Tafsiran larabci:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ
Na Akaifanya adhabu hiyo iwe ni mazingatio na ni onyo kwa watu mfano wake kati ya wale waasi. Hakika Firauni na kile kilichompata cha adhabu ni mawaidha kwa mwenye kuwaidhika na kutishika.
Tafsiran larabci:
ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا
Je, kufufuliwa kwenu, enyi watu, baada ya kufa ni kugumu zaidi, katika vipimo vyenu, au ni kuumbwa kwa mbingu?
Tafsiran larabci:
رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Amezipanga juu yenu kama jengo. Na Ameinua sakafu yake angani, haina tofauti wala nyufa.
Tafsiran larabci:
وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا
Na Ameutia giza usiku wake kwa kutwa kwa jua lake. Na Ameweka wazi mchana wake kwa kuchomoza kwake.
Tafsiran larabci:
وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Na ardhi baada ya kuumba mbingu Ameitandaza. Na Ameweka humo manufaa yake.
Tafsiran larabci:
أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا
Na Ametumbua humo chemchemu za maji. Na Ameotesha humo mimea inayolishwa.
Tafsiran larabci:
وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا
Na Ameyakita humo majabali yakiwa ni vigingi vyake. Ameumba, Aliyetakasika na kila upungufu,
Tafsiran larabci:
مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
neema zote hizi zikiwa ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu. (Hakika kurudisha kuumbwa kwenu, Siku ya Kiyama, ni sahali kwa Mwenyezi Mungu kushinda kuumba viumbe hivyo vyingine. Na vyote hivyo, kwa Mwenyezi Mungu, ni rahisi na ni vipesi).
Tafsiran larabci:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Pindi kitakapokuja Kiyama Kikubwa na balaa nzito, nao ni Mvuvio wa pili. Kipindi hicho zitaoneshwa kwa binadamu vitendo vyake vyote, za kheri na za shari.
Tafsiran larabci:
يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ
Hapo atazikumbuka na kuzitambua.
Tafsiran larabci:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Na utaoneshwa Moto wa Jahanamu kwa kila aonaye, uwe waonekana waziwazi.
Tafsiran larabci:
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Ama yule atakayekiuka amri ya Mwenyezi Mungu
Tafsiran larabci:
وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
na akapendelea maisha ya ulimwenguni kuliko ya Akhera,
Tafsiran larabci:
فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
basi kwa kweli marejeo yake ni Motoni.
Tafsiran larabci:
وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ
Na ama yule atakayeogopa kusimama mbele ya Mwenyezi Mungu kuhesabiwa na akaikanya nafsi yake na matamanio mapotofu,
Tafsiran larabci:
فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
basi Peponi ndiko makazi yake.
Tafsiran larabci:
يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا
Wanakuuliza washirikina, ewe Mtume, kwa madharau, kuhusu wakati wa kuanzia Kiyama unachowaonya.
Tafsiran larabci:
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ
Wewe huna kamwe ujuzi nacho.
Tafsiran larabci:
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Bali mambo ya ujuzi huo yarejeshwe kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye Sifa Tukufu.
Tafsiran larabci:
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا
Wewe linalokuhusu katika habari zake ni kumuonya nacho yule anayekiogopa.
Tafsiran larabci:
كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا
Kama kwamba wao siku watakapouona Kiyama kimesimama, watakuwa hawakukaa katika maisha yao ya duniani, kwa vituko vya hiko Kiyama, isipokuwa ni kama kwamba wamkaa kati ya adhuhuri mpaka kutwa juwa, au ni kama kati ya kuchomoza jua mpaka nusu ya mchana.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Sura: Suratu Al'nazi'at
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da yaren Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Rufewa