وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - عبد الله محمد و ناصر خميس * - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان


وه‌رگێڕانی ماناكان سوره‌تی: سورەتی البلد   ئایه‌تی:

Surat Al-Balad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mji huu mtakatifu wa Makkah.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Na wewe, ewe Nabii, ni mkazi wa mji huu mtakatifu.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na Anaapa kwa mzazi wa wanaadamu, ambaye ni Ādam, amani imshukie, na kilichozalikana na yeye.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika Tumemuumba binadamu katika usumbufu na shida za kilimwengu.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Kwani anadhani kwa mali aliyoyakusanya kuwa Mwenyezi Mungu Hatakuwa na uwezo juu yake?
تەفسیرە عەرەبیەکان:
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Huwa akisema kwa kujigamba: «Nimetumia mali mengi.»
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Kwani anadhani, kwa kitendo chake hiko, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda, Hamuoni wala hatamhesabu juu ya kubwa na dogo?
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili ya kuonea,
تەفسیرە عەرەبیەکان:
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
ulimi na midomo miwili ya kusemea
تەفسیرە عەرەبیەکان:
وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
na kumfafanulia njia mbili: ya kheri na ya shari?
تەفسیرە عەرەبیەکان:
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Basi ajiepushe na janga la Akhera kwa kutoa mali yake ili aokoke.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Ni kitu gani kilichojulisha ni lipi hilo janga la Akhera na ni mambo gani yenye kusaidia kujiepusha nalo?
تەفسیرە عەرەبیەکان:
فَكُّ رَقَبَةٍ
Ni kuacha huru shingo iliyoamini kuikomboa na utumwa.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kulisha, wakati wa shida ya njaa,
تەفسیرە عەرەبیەکان:
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
yatima mwenye ujamaa, ili ipatikane fadhila ya sadaka na ya kuunga kizazi,
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
au masikini asiyekuwa na kitu.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Kisha akawa, baada ya kufanya amali njema zilizotajwa, ni miongoni mwa waliotakasa Imani yao kwa Mwenyezi Mungu, wakausiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu kwa kufuata maamrisho Yake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi na wakausiana kuwahurumia viumbe.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Wenye kufanya hayo ndiwo watu wa kulia ambao watapelekwa Siku ya Kiyama upande wa kulia kuelekea Peponi.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Na wale waliokanusha Qur’ani ndio ambao watapelekwa, Siku ya Kiyama, upande wa kushoto kuelekea Motoni.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Malipo yao ni Moto wa Jahanamu wenye kuwafinika na kuwaziba.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
 
وه‌رگێڕانی ماناكان سوره‌تی: سورەتی البلد
پێڕستی سوره‌ته‌كان ژمارەی پەڕە
 
وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - عبد الله محمد و ناصر خميس - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان

وەرگێڕاوی ماناکانی قورئانی پیرۆز بۆ زمانی سواحیلی، وەرگێڕان: د. عبد الله محمد أبو بكر و شيخ ناصر خميس.

داخستن