クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 章: 町章   節:

Surat Al-Balad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mji huu mtakatifu wa Makkah.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Na wewe, ewe Nabii, ni mkazi wa mji huu mtakatifu.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na Anaapa kwa mzazi wa wanaadamu, ambaye ni Ādam, amani imshukie, na kilichozalikana na yeye.
アラビア語 クルアーン注釈:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika Tumemuumba binadamu katika usumbufu na shida za kilimwengu.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Kwani anadhani kwa mali aliyoyakusanya kuwa Mwenyezi Mungu Hatakuwa na uwezo juu yake?
アラビア語 クルアーン注釈:
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Huwa akisema kwa kujigamba: «Nimetumia mali mengi.»
アラビア語 クルアーン注釈:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Kwani anadhani, kwa kitendo chake hiko, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda, Hamuoni wala hatamhesabu juu ya kubwa na dogo?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili ya kuonea,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
ulimi na midomo miwili ya kusemea
アラビア語 クルアーン注釈:
وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
na kumfafanulia njia mbili: ya kheri na ya shari?
アラビア語 クルアーン注釈:
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Basi ajiepushe na janga la Akhera kwa kutoa mali yake ili aokoke.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Ni kitu gani kilichojulisha ni lipi hilo janga la Akhera na ni mambo gani yenye kusaidia kujiepusha nalo?
アラビア語 クルアーン注釈:
فَكُّ رَقَبَةٍ
Ni kuacha huru shingo iliyoamini kuikomboa na utumwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kulisha, wakati wa shida ya njaa,
アラビア語 クルアーン注釈:
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
yatima mwenye ujamaa, ili ipatikane fadhila ya sadaka na ya kuunga kizazi,
アラビア語 クルアーン注釈:
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
au masikini asiyekuwa na kitu.
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Kisha akawa, baada ya kufanya amali njema zilizotajwa, ni miongoni mwa waliotakasa Imani yao kwa Mwenyezi Mungu, wakausiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu kwa kufuata maamrisho Yake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi na wakausiana kuwahurumia viumbe.
アラビア語 クルアーン注釈:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Wenye kufanya hayo ndiwo watu wa kulia ambao watapelekwa Siku ya Kiyama upande wa kulia kuelekea Peponi.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Na wale waliokanusha Qur’ani ndio ambao watapelekwa, Siku ya Kiyama, upande wa kushoto kuelekea Motoni.
アラビア語 クルアーン注釈:
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Malipo yao ni Moto wa Jahanamu wenye kuwafinika na kuwaziba.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 町章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる