แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุหัมหมัด และ นาศิรฺ เคาะมีสฺ * - สารบัญ​คำแปล


แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: ‘Abasa   อายะฮ์:

Surat Abasa

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Yalidhihiri mabadiliko na mkunjiko katika uso wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
na akapa nyongo kwa sababu ya kwamba Abdallah bin Ummi Maktum alimjilia akitaka aelekezwe. Na alikuwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ameshughulika kuwalingania miamba wa Kikureshi katika Uislamu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Ni kitu gani kinakufanya wewe ujue uhakika wa jambo lake? Kwani huenda ikawa, kwa kuuliza kwake, nafsi yake itatakasika na kusafika.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au pengine apate mazingatio zaidi na kutishika.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Basi yule alijyejitosheleza na kutouhitajia uongozi wako,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
wewe ndiye unayemjali na wapulikiza maneno yake.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na ni kitu gani kinachokupa jukumu kwako iwapo hakusafika na ukafiri wake?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama yule ambaye amekuwa na pupa la kukutana na wewe,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
na huku anamuogopa Mwenyezi Mungu asiwe na kasoro katika kupata uongofu,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
wewe unampuuza. Ilivyotakikana ufanye si kama ulivyofanya, ewe Mtume.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Hakika Sura hii ni mawaidha kwako na kwa kila anayetaka kuwaidhika.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi atakaye atamkumbuka Mwenyezi Mungu na kumtaja na atafuata Wahyi Wake.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Wahyi huu, nao ni Qur’ani, uko katika kurasa zilizotukuzwa,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
zenye kuheshimiwa, zenye cheo cha juu,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
zilizosafishwa na uchafu, uongezaji na upunguzaji.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Zilizoko mikononi mwa Malaika waandishi, mabalozi kati ya Mwenyezi Mungu na viumbe Wake, wenye maumbile mema, tabia zao ni nzuri na njema na pia matendo yao.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Amelaaniwa mtu kafiri na ataadhibiwa. Ni uovu ulioje wa ukafiri wake kwa Mola wake!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwani hajui ni kwa kitu gani Mwenyezi Mungu Alimuumba kwacho mwanzo wake?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Mwenyezi Mungu Alimuumba kwa maji machache, nayo ni manii. Akayakadiria miongo yake.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha Akambainishia njia ya kheri na ya shari.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha humkosesha uhai, na Amemuekea mahali pa kuzikiwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha Akitaka Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na sifa mbaya, Atamhuisha na kumfufua baada ya kifo chake, kwa ajili ya kuhesabiwa na kulipwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
Mambo siyo kama yale anayoyasema kafiri na anayoyafanya. Bado hajatakeleza Aliyomuamrisha kwayo Mwenyezi Mungu katika kuamini na kutenda wema kwa kumtii.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Na azingatie binadamu, vipi Mwenyezi Mungu Amekiumba chakula chake ambacho ndicho kinachoendeleza maisha yake?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Aone kwamba Sisi Tumeyamimina maji ya mvua juu ya ardhi kwa wingi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Kisha Tumeipasua ardhi kwa Tulivyo vitoa kutoka humo miongoni mwa mimea tofauti.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Tukaotesha humo nafaka
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
na zabibu, na nyasi za wanyama.Na mizaituni na mitende.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mabustani yenye miti mikubwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na matunda
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
na ndisha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Mnajistareheshea kwazo, nyinyi na wanyama wenu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Utakapokuja Ukelele wa Siku ya Kiyama, ambao utayatia uziwi, kwa kitisho chake, masikizi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku mtu atakapomkimbia, kwa kitisho cha Siku Hiyo, nduguye
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
na babake na mamake na
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
mkewe na wanawe.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mmoja Siku Hiyo, atakuwa na jambo litakalomzuia asishughulike na mwingine.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Nyuso za wenye neema, Siku Hiyo, zitakuwa ni zenye kung’ara,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
zenye furaha na nderemo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso za watu wa Motoni zitakuwa na giza,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
nyeusi, zafinikwa na unyonge.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao wenye kusifika na sifa hiyo ndiwo wale waliozikufuru neema za Mwenyezi Mungu na wakazikanusha aya zake na wakayakeuka Aliyoyaharamisha kwa kutenda maovu na kukiuka mipaka.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: ‘Abasa
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุหัมหมัด และ นาศิรฺ เคาะมีสฺ - สารบัญ​คำแปล

แปลความหมายอัลกุรอานเป็นภาษาสวาฮิลีโดย ดร.อับดุลลอฮ์ มุฮัมหมัด อบูบักร และ ชัยค์ นาศิร เคาะมีส

ปิด