แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุหัมหมัด และ นาศิรฺ เคาะมีสฺ * - สารบัญ​คำแปล


แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Al-Inshiqāq   อายะฮ์:

Surat Al-Inshiqaq

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتۡ
Pindi mbingu itakapopasuka na kudhihiri mawingu katika pasuko zake Siku ya Kiyama.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ipasuke, na inastahili kufuata amri hiyo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ
Na pindi ardhi itakapotandikwa na kukunjuliwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ
Na milima yake kuvunjwa-vunjwa Siku hiyo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ifanye hivyo, na inastahili kufuata amri hiyo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدۡحٗا فَمُلَٰقِيهِ
Ewe binadamu, wewe unaenda kwa Mwenyezi Mungu na unafanya amali nzuri na mbaya, kisha utakutana na Yeye Siku ya Kiyama. Na huna budi kupata kutoka Kwake malipo mazuri zaidi ya amali yako njema au yanayolingana na amali yako mbaya.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ
Yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa mkono wake wa kulia,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا
naye ni yule aliyemuamini Mola wake, atahesabiwa hesabu pesi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا
Na atarudi kwa watu wake Peponi akiwa ni mwenye furaha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ
Na yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa nyuma ya mgongo wake,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا
naye ni yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu, ataita maangamvu na hasara,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَيَصۡلَىٰ سَعِيرًا
na ataingia Motoni.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّهُۥ كَانَ فِيٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورًا
Hakika yeye alikuwa kwa watu wake ulimwenguni ni mwenye furaha na majivuno, hafikirii mwisho wake utakuwa namna gani.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ
Alidhani hatarudi kwa Muumba wake, akiwa hai, kwa kuhesabiwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
بَلَىٰٓۚ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرٗا
Sivyo hivyo! Mwenyezi Mungu Atamrudisha kama alivomuumba na kumlipa kwa amali zake. Kwani Yeye kwake ni Mtambuzi na kwa hali yake ni Mjuzi kuanzia Alipomuumba mpaka kumfufua.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلشَّفَقِ
Mwenyezi Mungu Ameapa kwa wekundu wa pambizo za mbingu wakati wa kutwa jua.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلَّيۡلِ وَمَا وَسَقَ
Na kwa usiku na viunbe tofauti - tofauti vya kutambaa, kuruka na kutembea kwa miguu, uliokusanya.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ
Na kwa mwezi ukamilikapo mwangaza wake.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَتَرۡكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٖ
Mtapitia, enyi watu, miongo mbalimbali na hali tofauti : kutoka kwenye tone la manii, kuptia pande la damu, nofu la nyama hadi kutiwa roho, mpaka kufa na mpaka kufufuliwa. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, afanyapo hilo atakuwa ameingia kwenye ushirikina.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَمَا لَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Ni kitu gani kinachowazuia kumwamini baada ya aya zake kufafanuliwa kwao?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقُرۡءَانُ لَا يَسۡجُدُونَۤ۩
Na wana nini wao wanaposomewa Qur’ani hawamsujudii Mwenyezi Mungu wala hawajisalimishi kufuata yaliyokuja ndani yake?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُكَذِّبُونَ
Hakika tabia ya waliokufuru ni kuikanusha na kuikataa haki.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يُوعُونَ
Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa ukaidi wao wanaouficha kwenye nyoyo zao hali wao wanajua kuwa yale yaliyoletwa na Qur’ani ni kweli.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Basi wape bishara, ewe Mtume, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Amewaandalia adhabu yenye uchungu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونِۭ
Lakini wale wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakatekeleza amri waliyofaradhiwa na Mwenyezi Mungu watakuwa na malipo, Siku ya Akhera, yasiyokatika wala kupungua.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Al-Inshiqāq
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุหัมหมัด และ นาศิรฺ เคาะมีสฺ - สารบัญ​คำแปล

แปลความหมายอัลกุรอานเป็นภาษาสวาฮิลีโดย ดร.อับดุลลอฮ์ มุฮัมหมัด อบูบักร และ ชัยค์ นาศิร เคาะมีส

ปิด