Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-Tariq   Câu:

Surat At-Tariq

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu na nyota yenye kuchomoza usiku.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ
Na ni lipi lilokujulisha ni ukubwa gani wa nyota hiyo?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ
Hiyo ni nyota ing’arao na kuzagaa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ
Hakuna nafsi yoyote isipokuwa amewakilishwa kwayo Malaika mwenye kuchunguza na kusjili amali zake ili ihesabiwe Siku ya Kiyama.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Basi aangalie binadamu mwenye kukanusha kufufuliwa ameumbwa kwa kitu gani? Ili ajue kuwa kurudisha umbo lake mara ya pili si vigumu kama kuumbwa mara ya kwanza.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ
Aliumbwa kwa manii yenye kupenyeza ndani ya uzao kwa haraka.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yatokayo kwenye mgongo wa mwnamume na kifua cha mwanamke.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ
Hakika yule Aliyemuumba binadamu kwa maji haya ni muweza wa kumrudisha kwenye uhai baada ya kufa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ
Siku zitakapofunuliwa wazi siri ziliofichwa na nafsi na kupambanuliwa njema na mbovu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ
Binadamu hatakuwa na nguvu ya kuitetea nafsi yake wala hatakuwa na mtetezi wa kumwepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ
Na Anaapa kwa mbingu yenye mvua ya kukaririka.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلۡأَرۡضِ ذَاتِ ٱلصَّدۡعِ
Na ardhi yenye pasuko za kufanya mimea ichipuke.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلٞ فَصۡلٞ
Hakika Qur’ani ni neno lenye kupambanua baina ya haki na batili.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَمَا هُوَ بِٱلۡهَزۡلِ
Na si upuuzi. Haifai kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Akifanya hivyo atakuwa amemshirikisha Mwenyezi Mungu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّهُمۡ يَكِيدُونَ كَيۡدٗا
Hakika wenye kumkanusha Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani wanafanya vitimbi na mipango ili kuipinga haki na kuitilia nguvu batili.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَأَكِيدُ كَيۡدٗا
Na Mimi nafanya vitimbi kuidhihirisha haki ingawa makafiri wanatukia.Usiwe na haraka nao, ewe Mtume, kutaka wateremshiwe adhabu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَمَهِّلِ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَمۡهِلۡهُمۡ رُوَيۡدَۢا
Wape muhula uwangojee muda mchache wala usiwafanyie haraka, utaona adhabu itakayowafikia, mateso na maangamivu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-Tariq
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại