የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል ዐለቅ   አንቀጽ:

Surat Al-Alaq

ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ
Soma, ewe Nabii, Qur’ani uliyoteremshiwa ukianza kwa Jina la Mola wako Aliyepwekeka kwa kuumba.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ
Aliyemuumba kila binadamu kwa pande la damu nzito nyekundu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ
Soma, ewe Nabii, kile ulichoteremshiwa, na Mola wako ni Mwingi wa wema, Mwingi wa ukarimu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ
Aliyewafundisha viumbe vyake kuandika kwa kalamu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ
Alimfundisha binadamu vitu ambavyo hakuwa akivijua. Akamtoa kwenye giza la ujinga, Akampeleka kwenye nuru ya elimu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ
Kweli, binadamu hukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ
akijiona ametosheka kwa utajiri wake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ
Basi, ajue kila mwenye kutupa mipaka kuwa mwisho atarudi kwa Mwenyezi Mungu Ambaye Atamlipa kila binadamu kwa alilolitenda.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ
Je, umeona ujeuri wa ajabu zaidi kuliko wa mtu huyu, Abu jahl,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ
Anayemkataza mja wetu, Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, anapomsalia Mola wake?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ
Waonaje iwapo mwenye kukatazwa kusali yuko uongofuni, vipi anamkataza?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَوۡ أَمَرَ بِٱلتَّقۡوَىٰٓ
Au iwapo anaamrisha mwigine kumcha Mungu, vipi anamkataza hilo?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَرَءَيۡتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ
Waonaje iwapo huyu mwenye kukataza anakanusha lile alinganiwalo kwalo na kulipa mgongo,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ
hajui kuwa Mwenyezi Mungu anaona kila analolifanya?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّا لَئِن لَّمۡ يَنتَهِ لَنَسۡفَعَۢا بِٱلنَّاصِيَةِ
Basi mambo si kama anvyodai Abu Jahl. Na asipokomeka na ushindani alionao na udhia wake, Tutamshika upaa wake kwa nguvu na kumtia Motoni.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
نَاصِيَةٖ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٖ
Upaa wake ni upaa wenye maneno ya urongo na vitendo vya makosa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ
Basi na awalete, mtupaji mipaka huyu, watu wa baraza ili wamsaidiye.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ
Sisi Tutawaita Malaika wa adhabu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩
Mambo si kama Abu Jahl anavyoyadhania. Yeye, ewe Mtume, hawezi kukufanya lolote la kukudhuru Usimfuate kwa lile alilokuitia la kuwa uache Swala, bali msujudie Mola wako na uwe karibu na Yeye kwa kujipendekeza Kwake kwa kumtii.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል ዐለቅ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዶ/ር ሙሐመድ ዓብደሏህ አቡ በክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ

መዝጋት