Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-'Alaq   Câu:

Surat Al-Alaq

ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ
Soma, ewe Nabii, Qur’ani uliyoteremshiwa ukianza kwa Jina la Mola wako Aliyepwekeka kwa kuumba.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ
Aliyemuumba kila binadamu kwa pande la damu nzito nyekundu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ
Soma, ewe Nabii, kile ulichoteremshiwa, na Mola wako ni Mwingi wa wema, Mwingi wa ukarimu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ
Aliyewafundisha viumbe vyake kuandika kwa kalamu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ
Alimfundisha binadamu vitu ambavyo hakuwa akivijua. Akamtoa kwenye giza la ujinga, Akampeleka kwenye nuru ya elimu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ
Kweli, binadamu hukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ
akijiona ametosheka kwa utajiri wake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ
Basi, ajue kila mwenye kutupa mipaka kuwa mwisho atarudi kwa Mwenyezi Mungu Ambaye Atamlipa kila binadamu kwa alilolitenda.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ
Je, umeona ujeuri wa ajabu zaidi kuliko wa mtu huyu, Abu jahl,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ
Anayemkataza mja wetu, Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, anapomsalia Mola wake?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ
Waonaje iwapo mwenye kukatazwa kusali yuko uongofuni, vipi anamkataza?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَوۡ أَمَرَ بِٱلتَّقۡوَىٰٓ
Au iwapo anaamrisha mwigine kumcha Mungu, vipi anamkataza hilo?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَرَءَيۡتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ
Waonaje iwapo huyu mwenye kukataza anakanusha lile alinganiwalo kwalo na kulipa mgongo,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ
hajui kuwa Mwenyezi Mungu anaona kila analolifanya?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَلَّا لَئِن لَّمۡ يَنتَهِ لَنَسۡفَعَۢا بِٱلنَّاصِيَةِ
Basi mambo si kama anvyodai Abu Jahl. Na asipokomeka na ushindani alionao na udhia wake, Tutamshika upaa wake kwa nguvu na kumtia Motoni.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
نَاصِيَةٖ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٖ
Upaa wake ni upaa wenye maneno ya urongo na vitendo vya makosa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ
Basi na awalete, mtupaji mipaka huyu, watu wa baraza ili wamsaidiye.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ
Sisi Tutawaita Malaika wa adhabu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩
Mambo si kama Abu Jahl anavyoyadhania. Yeye, ewe Mtume, hawezi kukufanya lolote la kukudhuru Usimfuate kwa lile alilokuitia la kuwa uache Swala, bali msujudie Mola wako na uwe karibu na Yeye kwa kujipendekeza Kwake kwa kumtii.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-'Alaq
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại