Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Surah: Surah Az-Zalzalah   Ayah:

Surat Az-Zalzalah

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا
Itakapotikiswa ardhi mtikiso wa nguvu.
Tafsir berbahasa Arab:
وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا
Na ikatoa vilivyomo ndani yake: wafu na makandi.
Tafsir berbahasa Arab:
وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا
Na akauliza binadamu, kwa babaiko, «Imezukiwa na nini?»
Tafsir berbahasa Arab:
يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا
Siku ya Kiyama ardhi itatoa habari ya mambo iliyofanyiwa ya uzuri na ubaya.
Tafsir berbahasa Arab:
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا
kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Ameiamuru itoe habari ya mambo iliyofanyiwa.
Tafsir berbahasa Arab:
يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Siku hiyo wataondoka kutoka kwenye kisimamo cha Hesabu wakiwa makundi, ili Mwenyezi Mungu Awaoneshe waliyoyatenda, mazuri na mabaya, na Awalipe kwayo.
Tafsir berbahasa Arab:
فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ
Yoyote mwenye kufanya jema wezani wa chungu mdogo atayaona malipo yake Akhera.
Tafsir berbahasa Arab:
وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ
Na yoyote mwenye kufanya baya wezani wa chungu mdogo atayaona malipo yake Akhera.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Surah: Surah Az-Zalzalah
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Terjemahan makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke bahasa Sawahili oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis

Tutup