Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: Al-Mā‘ūn   Ayah:

Al-Ma'un

أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يُكَذِّبُ بِٱلدِّينِ
Je, waiona hali ya yule ambaye akanusha kufufuliwa na kulipwa?
Arabic explanations of the Qur’an:
فَذَٰلِكَ ٱلَّذِي يَدُعُّ ٱلۡيَتِيمَ
Huyo ndiye yule anayemkaripia yatima kwa nguvu akimnyima haki yake kwa sababu ya ususuavu wa moyo wake.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Na wala hawahimizi wengine kulisha masikini. Vipi yeye mwenyewe atamlisha?.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَوَيۡلٞ لِّلۡمُصَلِّينَ
Basi adhabu kali itawafikia wenye kusali,
Arabic explanations of the Qur’an:
ٱلَّذِينَ هُمۡ عَن صَلَاتِهِمۡ سَاهُونَ
ambao wameghafilika na Swala zao: hawazisimamishi kama ipasavyo wala hawazisali kwa nyakati zake.
Arabic explanations of the Qur’an:
ٱلَّذِينَ هُمۡ يُرَآءُونَ
Ambao huonyesha watu amali zao za kheri kwa njia ya ria.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَيَمۡنَعُونَ ٱلۡمَاعُونَ
Na wanakataa kuwaazima watu vitu ambavyo hawadhuriki kwa kuviazima, kama vyombo vya kutumia na vinginevyo. Wao hawakujifanyia wema nafsi zao kumuabudu Mola wao wala hawakuwafanyia wema viumbe Vyake.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Al-Mā‘ūn
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis - Translations’ Index

Translated by Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr & Sh. Naser Khamis

close