Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Simoore: Simoore al-Maawuun   Aaya:

Surat Al-Ma'un

أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يُكَذِّبُ بِٱلدِّينِ
Je, waiona hali ya yule ambaye akanusha kufufuliwa na kulipwa?
Faccirooji aarabeeji:
فَذَٰلِكَ ٱلَّذِي يَدُعُّ ٱلۡيَتِيمَ
Huyo ndiye yule anayemkaripia yatima kwa nguvu akimnyima haki yake kwa sababu ya ususuavu wa moyo wake.
Faccirooji aarabeeji:
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Na wala hawahimizi wengine kulisha masikini. Vipi yeye mwenyewe atamlisha?.
Faccirooji aarabeeji:
فَوَيۡلٞ لِّلۡمُصَلِّينَ
Basi adhabu kali itawafikia wenye kusali,
Faccirooji aarabeeji:
ٱلَّذِينَ هُمۡ عَن صَلَاتِهِمۡ سَاهُونَ
ambao wameghafilika na Swala zao: hawazisimamishi kama ipasavyo wala hawazisali kwa nyakati zake.
Faccirooji aarabeeji:
ٱلَّذِينَ هُمۡ يُرَآءُونَ
Ambao huonyesha watu amali zao za kheri kwa njia ya ria.
Faccirooji aarabeeji:
وَيَمۡنَعُونَ ٱلۡمَاعُونَ
Na wanakataa kuwaazima watu vitu ambavyo hawadhuriki kwa kuviazima, kama vyombo vya kutumia na vinginevyo. Wao hawakujifanyia wema nafsi zao kumuabudu Mola wao wala hawakuwafanyia wema viumbe Vyake.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simoore al-Maawuun
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude